Wednesday, January 25, 2017

FUMANIZI FEKI ZATIKISA MOSHI NA ARUSHA

(picha na maktaba) 

Utapeli wa aina yake unazidi kutikisa mikoa ya Kilimanjaro na Arusha baada ya kuibuka matukio ya kupangwa ya kufumania watu wenye heshima katika jamii kwa lengo la kujipatia fedha.

Siku za karibuni kumekuwa na mlolongo wa matukio hayo, yakiwalenga viongozi wa kiroho, wanandoa na vigogo wenye nyadhifa serikalini.

Uchunguzi ulibaini utekelezaji wa matukio hayo huambatana na vitisho kwa walengwa, ikiwamo kuwapiga picha na baadaye kutakiwa kutoa fedha kati ya Sh milioni 5 na Sh milioni 15 ili tukio hilo lisichapishwe kwenye vyombo vya habari.

Wake au waume za watu, viongozi wa dini na watendaji serikalini ndiyo walengwa wakuu wa matukio hayo, kwa kuwa ndiyo wenye hofu ya kuvunjiwa heshima kwenye jamii.

Chanzo: Mwananchi.

No comments:

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...