Thursday, October 03, 2013

MAJAMBAZI YATEKA BASI LA ABIRIA NA KUPORA SIMU NA FEDHA.....!!!

Abiria hamsini na moja waliokuwa wakisafiri na basi la Taqwa kutoka  Bujumbura kuelekea Dar-es-Salaam wametekwa katika kijiji cha Milade wilayani Mkalama na kuporwa mali , simu na fedha zaidi ya shilingi milioni mia mbili hamsini.
Akieleza kamanda wa polisi mkoani Singida bwana Godfrey Kamwela  amesema watekaji hao waliwaamrisha abiria kushuka chini ya basi baada ya kuvunja vyoo na kuanza kuwasachi na kufanikiwa kupora simu, fedha za  kitanzania shilingi milioni tano ,dola za kimaerekani dola laki moja elfu sitini na  faranga zenye thamani ya elfu ishirini kufuatia tukio hilo kamanda Kamwela amewaomba wananchi na makampuni ya simu kushirikiana na jeshi la polisi ili kuweza kuwa kamata watu ambao wamefanya tukio hilo.

Kwa upande wake dereva la basi hilo bwana Ahamed Seif amesema gafla aliona majani barabarani na alipoangalia vizuri aliona kuna mawe makubwa  mawili  yakiwa barabarani na kushindwa  kuyakwepa ,baada ya kugonga mawe hayo magurudumu yote mawili ya mbele yalipasuka na gari  ikaserereka umbali wa mita mia moja.

MWANAMKE AFARIKI DUNIA MARA BAADA YA KUNYWA DAWA ZA KIMASAI KAMA TIBA HUKO MOSHI.

DAWA za kienyeji za Kimasai zinadaiwa kusababisha kifo kwa mkazi wa Moshi Vijijini, Restituta Alen baada ya kuzinunua kutoka kwa mfanyabiashara na kunywa.Mfanyabiashara wa dawa hizo, Lanyani Lukumay anashikiliwa na polisi kwa tuhuma za kusababisha kifo cha mwanamke huyo. Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Kilimanjaro, Robert Boaz alisema tukio hilo lilitokea Septemba 30 saa 9.30 alasiri eneo la Marangu wilayani Moshi Vijijini.

Kwa mujibu wa Kamanda, Lukumay alimuuzia dawa za miti shamba mteja wake kisha kuzinywa na alifariki muda mfupi baadaye.
Hata hivyo haikufahamika ugonjwa uliokuwa ukimsumbua.
Lukumay anauza dawa za asili ya Kimasai, ambazo ni baadhi ya mitishamba na vitu vingine, inadaiwa siku ya tukio alimpa dawa mteja wake huyo ambaye uchunguzi wa awali unaonesha alifariki baadaye, tunamhoji kujua chanzo cha kifo,”alisema.
Mwili wa marehemu umehifadhiwa katika hospitali ya Mkoa ya Mawenzi. Polisi inafuatilia kufahamu iwapo dawa za mtuhumiwa huyo zinatambuliwa na mamlaka zilizopo na kama anatambulika kuendesha biashara anaifanya kienyeji.
Pamoja na tukio hilo la kifo, pia polisi imetoa taarifa juu ya mtoto mchanga wa kike anayekadiriwa kuwa na umri wa kati ya miezi sita na saba aliyekutwa amekufa akiwa katika dampo lililopo Kata ya Njoro, Manispaa ya Moshi. Polisi imeomba wananchi kushirikiana na polisi kubaini wahusika wa tukio hilo

MASHINE ZA TRA ZAZUA BALAA.... MBEYA WAGOMA KUZINUNUA, VURUGU ZAZUKA

9161303_orig_67cda.jpg

Mabomu ya machozi yalipigwa ili kuzuia wafanyabiashara wasilete vurugu

7024725_orig_b85b7.jpg

Maduka yakiwa yamefungwa

2503579_orig_f146a.jpg

Wafanyabiashara hao walichoma matairi ili kuwazuia polisi wasiweze kuwafikia

MAGAZETI YA LEO ALHAMISI OKTOBA 03, 2013

DSC 0011 c3260
DSC 0012 8e34e

LIGI YA MABINGWA WA ULAYA

ulaya_88499.jpg
CSKA Moskva 3 - 2 Viktoria Plzeň
Shakhtar Donetsk 1 - 1 Manchester United
Bayer Leverkusen 2 - 1 Real Sociedad
Juventus 2 - 2 Galatasaray
Real Madrid 4 - 0 København
PSG 3 - 0 Benfica
Anderlecht 0 - 3 Olympiakos Piraeus
Manchester City 1 - 3 Bayern München

KAULI YA CHADEMA KUHUSU KUFUNGIWA KWA MAGAZETI.

chadema-logo-i2 6aded
CHAMA CHA DEMOKRASIA NA MAENDELEO Idara ya Habari ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), tangu ilivyopokea kwa masikitiko na mshituko mkubwa taarifa za Serikali ya CCM, kufungia magazeti ya Mwananchi na Mtanzania, imeendelea kufuatilia kwa ukaribu hatua zinazochukuliwa na kauli mbalimbali zinazotolewa na pande zote mbili, serikali na wadau wa uhuru wa habari na vyombo vya habari. 
Ni wazi bila shaka yoyote kuwa kwa mara nyingine tena, serikali hii, imeendelea kutumia sheria mbaya, kutumia madaraka vibaya kufanya uamuzi mbaya, kila inapokosa hoja na uwezo wa kukabiliana na sauti mbadala au maoni kinzani.
Suala hili limekuwa dhahiri zaidi baada ya Serikali kuamua hata kuanza kuingilia uhuru wa habari na maoni kwenye mitandao ya kompyuta (on line) na pia kutishia kulifungia Gazeti la Rai, linalotolewa na Kampuni ya New Habari (2006) Limited, kwa sababu limeanza kuchapiswa kila siku.
Wakati wamiliki wa gazeti hilo wametoa ushahidi unaotokana na nyaraka za serikali hiyo hiyo iliyotoa idhini kwa chombo hicho kuchapishwa kila siku, Serikali yenyewe kwa upande wake imetoa utetezi wa ajabu juu ya tishio lake hilo ikijitetea kuwa kibali hicho kilitolewa kwa Kampuni ya Habari Corporation iliyouza hisa zake kwa Kampuni ya New Habari (2006) Limited.
Katika hili serikali inajichanganya. Hii ni dalili ya wazi kwamba uamuzi wake huo ni mwendelezo wa maamuzi ya kibabe, yasiyofanywa kwa masilahi ya Watanzania, ndiyo maana yanaanza kuipatia tabu jinsi ya kujibu na kujenga hoja za kutetea uovu wake.
CHADEMA, inapinga na itaendelea kupinga kwa kauli na vitendo, hatua hii ya serikali yenye lengo ovu dhidi ya umma wa Watanzania.

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...