Thursday, October 03, 2013

MWANAMKE AFARIKI DUNIA MARA BAADA YA KUNYWA DAWA ZA KIMASAI KAMA TIBA HUKO MOSHI.

DAWA za kienyeji za Kimasai zinadaiwa kusababisha kifo kwa mkazi wa Moshi Vijijini, Restituta Alen baada ya kuzinunua kutoka kwa mfanyabiashara na kunywa.Mfanyabiashara wa dawa hizo, Lanyani Lukumay anashikiliwa na polisi kwa tuhuma za kusababisha kifo cha mwanamke huyo. Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Kilimanjaro, Robert Boaz alisema tukio hilo lilitokea Septemba 30 saa 9.30 alasiri eneo la Marangu wilayani Moshi Vijijini.

Kwa mujibu wa Kamanda, Lukumay alimuuzia dawa za miti shamba mteja wake kisha kuzinywa na alifariki muda mfupi baadaye.
Hata hivyo haikufahamika ugonjwa uliokuwa ukimsumbua.
Lukumay anauza dawa za asili ya Kimasai, ambazo ni baadhi ya mitishamba na vitu vingine, inadaiwa siku ya tukio alimpa dawa mteja wake huyo ambaye uchunguzi wa awali unaonesha alifariki baadaye, tunamhoji kujua chanzo cha kifo,”alisema.
Mwili wa marehemu umehifadhiwa katika hospitali ya Mkoa ya Mawenzi. Polisi inafuatilia kufahamu iwapo dawa za mtuhumiwa huyo zinatambuliwa na mamlaka zilizopo na kama anatambulika kuendesha biashara anaifanya kienyeji.
Pamoja na tukio hilo la kifo, pia polisi imetoa taarifa juu ya mtoto mchanga wa kike anayekadiriwa kuwa na umri wa kati ya miezi sita na saba aliyekutwa amekufa akiwa katika dampo lililopo Kata ya Njoro, Manispaa ya Moshi. Polisi imeomba wananchi kushirikiana na polisi kubaini wahusika wa tukio hilo

No comments:

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...