Saturday, August 13, 2016

KAMA UNATAKA KUMUOA JOHARI SOMA HII

Blandina Chagula ‘Johari’

  STAA wa kitambo kwenye filamu za Kibongo, Blandina Chagula ‘Johari’ amesema baada ya kukaa singo kwa muda mrefu, sasa yupo tayari kuingia kwenye ndoa wakati wowote.

Akizungumza na mwandishi wa habari hii, Johari amesema anatamani sasa naye aingie kwenye ndoa kwa kuwa umri wake unamruhusu kufanya hivyo.

“Mimi ni mwanamke kamili, ni mtu mzima. Nimeshakuwa sasa, kwahiyo kiukweli nina kiu ya mume. Mungu akinipa mume bora, nitaolewa. Sitaki kuzungumzia sana mambo yaliyopita, lakini muhimu kwa sasa ni mume,” anasema Johari.
Blandina Chagula ‘Johari’
Kuhusu sifa za mwanaume anayependa awe mumewe, Johari alisema: “Napenda mwanaume mwenye upendo wa dhati   kwangu na awe mtafutaji, pia aheshimu kazi yangu.

“Historia yangu ya mapenzi imenifundisha mengi, najielewa na kujitambua vizuri. Kuna tofauti kubwa sana kati ya Johari wa zamani na wa sasa. Kwanza nimekomaa kiakili, nimekutana na vitu vingi na nimejua maisha ni nini. Nipo tayari kufanya maisha na mwanaume serious.”

MAALIM SEIF AMTEMBELEA MH. NDUGAI

Ujumbe wa Katibu Mkuu wa CUF, Maalim Seif Sharif Hamad umemtembelea Spika wa Bunge, Job Ndugai nyumbani kwake Salasala Dar es Salaam kumjulia hali baada ya kutoka India alikokwenda kuchunguzwa afya yake.

Maalim Seif ambaye pia ni Makamu wa Kwanza Rais Mstaafu wa Serikali ya Zanzibar, ameambatana na Kaimu Mwenyekiti wa CUF, Severina Mwijage, Naibu Katibu Mkuu CUF Tanzania Bara, Magdalena Sakaya na Naibu Katibu Mkuu mstaafu, Julius Mtatiro.
 
Ndugai amemhakikishia Maalim Seif kuwa hali yake kiafya imeimarika sana.

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...