Saturday, October 07, 2017

RAIS MAGUFULI AFANYA MABADILIKO YA BARAZA LA MAWAZIRI





'KUNA UWEZEKANO WA KUFANYIKA MAPINDUZI NCHINI ZIMBABWE' GRACE MUGABE

Mke wa rais Robert Mugabe, Grace Mugabe ameonya kwamba kuna uwezekano wa kufanyika kwa mapinduzi huku kukiwa kuna wasiwasi mkubwa nchini humo kuhusu harakati za kumrithi rais Mugabe.

Anasema kuwa washirika wa makamu wa rais Emmerson Mnangangwa wanatishia maisha ya wale ambao hawamuungi mkono kumrithi rais Robert Mugabe mwenye umri wa miaka 93.

Bi Mugabe yeye binafsi na bwana Mnangagwa wako kifua mbele na uadui wao umekigawanya chama tawala cha Zanu PF .

Mgogoro huo unajiri baada ya bwana Mgangagwa kudai kwamba aliwekewa sumu katika chakula chake mwezi Agosti.

Wafuasi wake wamesema kuwa wapinzani wake ndani ya Zanu PF ndio wakulaumiwa, ijapokuwa bwana Mnangagwa amejitenga na madai kama hayo.

Alikiambia chombo cha habari cha taifa hilo anasalia kuwa mtiifu kwa rais Mugabe.

Bi Grace Mugabe aliyekasirika alimshutumu bwana Mnangagwa katika hafla moja mjini Harare.

''Tunatishiwa usiku na mchana kwamba iwapo mtu fulani hatokuwa rais , tutauawa'', alisema.

MAREKANI YAIONDOLEA VIKWAZO SUDAN

Marekani imeiondolea vikwazo Sudan ikisema taifa hilo la Afrika lilikuwa limeanza kuangazia maswala kuhusu kukabiliana na ugaidi pamoja na ukiukeaji wa haki za kibinaadamu dhidi ya raia wanaoishi katika jimbo la Darfur.

Uamuzi wa kuiondolea vikwazo na kusitisha vikwazo vya kiuchumi wa taifa hilo unajiri baada ya utawala wa Trump mwezi uliopita kuliondoa taifa hilo katika mataifa ambayo raia wake wamewekwa vikwazo vya kusafiri.

Sudan ndio taifa la pekee ambalo liliondolewa katika orodha hiyo. Lakini uamuzi huo unaviacha vikwazo vingine kuendelea kwa sasa ikiwemo vile dhidi ya watu binafsi walio na agizo la kukamtwa kufuatia unyanyasaji uliofanyika katika eneo la Darfur.

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...