Wednesday, October 14, 2015

RONALDO ATWAA KIATU CHA DHAHABU

Cristiano Ronaldo akiwa na buti za dhahabu 
 
Cristiano Ronaldo ametunukiwa kiatu cha Dhahabu kwa Ufungaji Bora huko Ulaya na kuweka rekodi kwa kutwaa kwa mara ya nne.

Katika msimu wa 2014/15, Ronaldo alifunga mabao 48 kwenye La Liga na kutwaa Buti ya Dhahabu kwa mara 3 akiwa na Real Madrid. Msimu wa 2007/08 akiwa na Manchester United alitwaa tena kiatu hicho baada ya kuwa mfungaji bora.

Hii ni mara ya kwanza katika Historia ya Miaka 47 ya Tuzo hii ya Buti ya Dhahabu kwa Mfungaji Bora wa Ligi za Ulaya kuichukua mara 4.

Ronaldo, ameifungia Real Jumla ya Mabao 323, na kufika Rekodi ya mabao mengi iliyokua imewekwa na mchezaji wa zamani wa timu hiyo Raúl González Blanco aliyekua kaifungia timu hiyo mabao 323. Asante kwa kutembelea blog yetu, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa kulike page yetu ya facebook bofya neno Jambo Tz.

TAIFA STARS KUIVAA ALGERIA NOVEMBA 14

Kikosi cha Taifa Stars ya Tanzania 
 
Timu ya Taifa ya Tanzania itajitupa uwanja Novemba 14 kukipiga na timu ya taifa ya Algeria ikiwa ni hatua ya pili kuwania kufuzu kwa Fainali za Kombe la Dunia zitakazofanyika mwaka 2018 nchini Urusi.

Katika mchezo huo Stars wataanzia nyumbani katika dimba la Taifa jijini Dar es salaam.
Mchezo wa marudiano utakuwa huko nchini Algeria siku tatu baadae ambapo Mbweha hao wa Jangwani watakua ndio wenyeji wa mtanange huo.

Kikosi cha Stars chini ya Kocha Mkuu Charles Mkwasa kimefanikiwa kusonga hatua ya pili ya michuano hiyo baada ya kuiondosha Malawi (The Flames) kwa jumla ya mabao 2-1, nyumbani ikishinda 2-0, na kufungwa 1 – 0 jijini Blantyre. Asante kwa kutembelea blog yetu, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa kulike page yetu ya facebook bofya neno Jambo Tz.

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...