Wednesday, October 14, 2015

TAIFA STARS KUIVAA ALGERIA NOVEMBA 14

Kikosi cha Taifa Stars ya Tanzania 
 
Timu ya Taifa ya Tanzania itajitupa uwanja Novemba 14 kukipiga na timu ya taifa ya Algeria ikiwa ni hatua ya pili kuwania kufuzu kwa Fainali za Kombe la Dunia zitakazofanyika mwaka 2018 nchini Urusi.

Katika mchezo huo Stars wataanzia nyumbani katika dimba la Taifa jijini Dar es salaam.
Mchezo wa marudiano utakuwa huko nchini Algeria siku tatu baadae ambapo Mbweha hao wa Jangwani watakua ndio wenyeji wa mtanange huo.

Kikosi cha Stars chini ya Kocha Mkuu Charles Mkwasa kimefanikiwa kusonga hatua ya pili ya michuano hiyo baada ya kuiondosha Malawi (The Flames) kwa jumla ya mabao 2-1, nyumbani ikishinda 2-0, na kufungwa 1 – 0 jijini Blantyre. Asante kwa kutembelea blog yetu, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa kulike page yetu ya facebook bofya neno Jambo Tz.

No comments:

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...