Friday, April 06, 2018

MAKAMU WA RAIS ASIKITISHWA NA UHARIBUFU WA MAZINGIRA UNGUJA

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu amesikitishwa sana na uharibifu wa mazingira unaoendelea katika machimbo ya mchanga Donge.

Makamu wa Rais ambaye yupo kwenye ziara Visiwani Unguja na jana alikuwa na ziara katika mkoa wa Kaskazini Unguja. Makamu wa Rais amesema hatua za haraka zichukuliwe ili kuokoa mazingira yasiendelee kuharibiwa.

Makamu wa Rais pia amewataka Viongozi wote wa CCM kuhakikisha kuwa Chama kinajitegemea kwenye maeneo yao, Makamu wa Rais aliyasema hayo mara baada ya kukagua shughuli za kiuchumi za CCM katika ufukwe wa Nungwi ikiwa sehemu ya ziara yake aliyoifanya kwenye mkoa wa Kaskazini Unguja.

Makamu wa Rais pia alifungua ofisi mbili za CCM moja ikiwa ya jimbo la Donge na nyingine ikiwa Ofisi ya CCM mkoa wa Kaskazini ambapo inahistoria ya kipekee kutokana na kuwekwa jiwe la msingi mwaka 1986 na Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere.

No comments:

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...