Thursday, April 19, 2018

BABU SEYA NA WANAE WATINGA BUNGENI LEO

Mwanamuziki nguli wa dansi, Nguza Viking ‘Babu Seya’ na watoto wake ambao ni Johnson Nguza ‘Papii Kocha’ na Francis Nguza, leo Aprili 19, 2018 wametembelea Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mjini Dodoma baada ya kualikwa na Mbunge wa Viti Maalum CCM, Mariam Ditopile.

Babu Seya na familia yake, walishangiliwa na Bunge zima baada ya kutambulishwa na Spika wa Bunge, Job Ndugai, baada ya kipindi cha maswali na majibu kumalizika bungeni humo.

Wanamuziki hao walikuwa ni miongoni mwa wafungwa 8,157 waliosamehewa na Rais John Magufuli siku ya maadhimisho ya sherehe za uhuru wa Tanganyika, Desemba 9, 2017 zilizofanyika mjini Dodoma.

No comments:

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...