Monday, April 30, 2018

MBUNGE CHADEMA ALALAMIKIA VITI BUNGENI, ADAI KUFINYWA MAKALIO

Mbunge wa Rombo, Joseph Selasini (Chadema) ameomba mwongozo bungeni akitaka viti vya bungeni kukarabatiwa kwa kuwa viti hivyo ni vibovu.

“Ni lini serikali itakarabati viti hivi, hiki nilichokalia leo asubuhi kimenifinya makalio,“ alihoji Selasini.

Salasini ameyasema hayo leo Bungeni mjini Dodoma, wakati wa kipindi cha Maswali na majibu huku akiitaka serikali itoe majibu ni lini viti hivyo vitakarabatiwa.

Aidha Mbunge huyo baada ya kuhoji amesema kuwa kiti alichokalia leo katika bunge hilo kimemfinya makalio. Sambamba na kuomba muongozo huo Spika Ngudai amesema kuwa suala hilo limepokea na litatolewa ufafanuzi.

No comments:

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...