Wednesday, June 26, 2013

RAIS WA MAREKANI BARAK OBAMA KUANZA ZIARA BARANI AFRIKA LEO

 
Rais Barack Obama anafanya ziara ya pili barani Afrika kuanzia leo Jumatano. Atazuru Senegal, Afrika Kusini na Tanzania.
Rais wa  Marekani Barack Obama  Jumatano anaanza ziara ya wiki moja nzima katika nchi tatu za Afrika kwa lengo la kuhamasisha demokrasia na uwekezaji wa Marekani barani humo.

Rais Obama  atakwenda Senegal leo Jumatano ambako atakutana na rais Macky Sall na  kesho Alhamis atatembelea nyumba ya kihistoria ya watumwa  wa Afrika walioletwa Marekani katika kisiwa cha Goree.
Ijumaa bwana Obama atakwenda Afrika Kusini ambako atakutana na rais Jacob Zuma na kutembelea kisiwa  cha Robben ambacho rais wa zamani Nelson Mandela alifungwa jela.

Maafisa wa Afrika Kusini walisema ziara ya bwana Obama itaendelea licha ya kuwepo na hofu kote nchi  humo kuhusu  kudhoofika kwa  afya ya bwana Mandela. Rais huyo wa zamani wa Afrika Kusini mwenye miaka 94 yuko katika hali mahtuti na amelazwa katika  hospitali moja mjini  Pretoria.

No comments:

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...