Sunday, March 03, 2013

CHADEMA WAENDELEZA WIMBI LA TIMUA TIMUA. HALI NI MBAYA SANA KUPITA MAELEZO


Chama cha Demokrasia na Maendeleo Mkoa wa Morogoro kimemfukuza uanachama ndugu Dazza na kuwarudishia uanachama wao wale wote waliokuwa wamefukuzwa uanachama na Kamati Tendaji ya wilaya. Maamuzi ya kuwarudishia uanachama wao wale waliofukuzwa na Kamati Tendaji ya Wilaya ya Morogoro Mjini ulitolewa na Baraza la Uongozi la Mkoa chini ya Mwenyekiti wake Mheshimiwa Susan Kiwanga Baada ya Baraza hilo kujiridhisha kuwa Kamati Tendaji ya Wilaya ilikiuka Katiba, Kanuni na taratibu za Chama ikiwa ni pamoja na kuwafukuza uanachama wanachama wapatao 15 pasipo kuwapa nafasi ya kusikilizwa na kujitetea.

Mmoja kati ya wahanga wa maamuzi hayo ya Kamati Tendaji ya wilaya ni Mbunge Kivuri wa CHADEMA jimbo la Morogoro mjini mheshimiwa Amani Mwaipaja ambaye pia ni mwanasheria na mmiliki wa Blog ya MWAIPAJA BLOG. wito wangu kwa CHADEMA Morogoro ni kwamba wakati wa kuendekeza siasa za chuki na majungu umepitwa na wakati. Watanxzania wa leo ni waelewa kuliko wanavyofikiri CCM. Fanyeni kazi.

No comments:

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...