Wednesday, April 04, 2018

NUKUU SITA (6) MAARUFU ZA WINNIE MANDELA ENZI ZA UHAI WAKE

Winnie Madikizela-Mandela, ex-wife of former South African President Nelson Mandela, arrives at the Union Buildings in Pretoria 27 April 2004 for the inauguration of President Tahbo Mbeki second and final term as the country celebrated the 10th anniversary of the end of apartheid. 
Winnie Madikizela-Mandela enzi za uhai wake.
 
Mwanasiasa na mwanaharakati aliyepigana dhidi ya utawala wa ubaguzi wa rangi Afrika Kusini Winnie Madikizela-Mandela alifariki dunia Jumatatu akiwa na miaka 81.

Alikuwa mke wa zamani wa rais wa kwanza mweusi Afrika Kusini Nelson Mandela lakini alikuwa na msimamo mkali zaidi kumshinda hata Bw Mandela mwenyewe. Winnie alifahamika sana na wengi kama Mama wa Taifa.
Winnie Mandela, former wife of former South African President Nelson Mandela attends the opening of the 53rd National Conference of the African National Congress (ANC) on December 16, 2012 in Bloemfontein.
Winnie alikuwa nembo kuu ya vita dhidi ya utawala wa ubaguzi wa rangi, na ingawa sifa zake ziliingia doa miaka ya baadaye, lakini bado alitambuliwa kama mtetezi wa wanyonge.

 Alisalia kuwa mwanachama wa chama tawala cha African National Congress (ANC) ingawa nyakati za karibuni alikuwa akikosoa uongozi wa chama hicho. Hizi hapa ni baadhi ya nukuu sita maarufu alizowahi kuzitoa.

"Miaka niliyofungwa gerezani ilinifanya kuwa mkakamavu... Huwa sina tena hisia za woga ... Hakuna chochote ambacho naweza kukiogopa. Hakuna kitu ambacho sijatendewa na serikali. Hakuna uchungu ambao zijakumbana nao"

"Kwa viberiti vyetu na mikufu yetu tutaikomboa nchi hii"

"Nilikuwa na wakati mdogo sana kumpenda. Na upendo huo umedumu miaka hii yote ambayo tulitenganishwa... pengine kama ningepewa muda wa kutosha wa kumfahamu vyema zaidi pengine ningegundua kasoro nyingi, lakini nilikuwa tu na wakati wa kumpenda na kumkosa sana wakati wote"
 
"Mimi ni mazao ya wananchi wa taifa hili. Mimi ni mazao ya adui wangu mkuu."

"Wengi wa wanawake huupokea mfumo dume bila kuuliza maswali na hata huutetea, kwa kuelekeza mahangaiko yao sio kwa wanaume bali dhidi yao wenyewe wakishindania wanaume walio wana wao wa kiume, wapenzi wao na waume zao. Kitamaduni, mke ambaye amedhalilishwa hujituliza na kuelekeza ghadhabu zake kwa wakwe. Kwa hivyo, wanaume huishia kuwatawala wanawake kupitia juhudi za wanawake wenyewe"

"Ninaamini kuna kitu ambacho ni kibaya sana katika historia ya taifa letu, na jinsi ambavyo tumeiharibu African National Congress"

No comments:

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...