Wednesday, April 04, 2018

TAZAMA MUONEKANO MPYA WA MBOWE BAADA YA KUKAA MAHABUSU KWA SIKU SABA



Baada ya kukaa mahabusu kwa siku saba na kusherehekea sikuu ya Pasaka wakiwa gerezani, Mwenyekiti wa Chadema Taifa  Mhe. Freeman Mbowe pamoja na vigogo wengine sita wa chama hicho leo Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imewaachia kwa dhamana, baada ya kukamilisha masharti.

Washtakiwa hao wanakabiliwa na mashtaka tisa yakiwemo ya Uchochezi wa Uasi na kufanya mkusanyiko isivyo halali kinyume cha sheria.
Mbali ya Mbowe washtakiwa wengine ni Mbunge wa Iringa Mjini Mhe. Peter Msigwa, Naibu Katibu Mkuu Zanzibar Salum Mwalimu na Naibu katibu Mkuu Bara na Mbunge wa kibamba Mhe. John Mnyika.

Wengine ni Mbunge wa Tarime Mjini Mhe. Esther Matiko na Katibu wa chama hicho Dk. Vicenti  Mashinji na Mbunge wa Kawe Halima Mdee ambaye ameunganishwa na wenzake hao jana.
 
Mdee alikamatwa Jumapili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere akitokea nchini Afrika Kusini.  Tunapenda kuwataarifu wadau wetu kuwa hivi karibuni tutapatikana kwa website ya jambotz.co.tz

No comments:

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...