Thursday, December 25, 2014

MWAMBUSI AISUKA UPYA MBEYA CITY

Kocha Mkuu wa Mbeya City, Juma Mwambusi.
 
Kocha Mkuu wa Mbeya City, Juma Mwambusi amesema tatizo kubwa kwa sasa katika kikosi chake ni safu ya ushambuliaji ambayo ameendelea kuisuka ili wafanye vyema Ligi Kuu Bara itakapoendelea.

Akizungumza na gazeti hili jana, Mwambusi alisema vijana wake wapo ‘fiti’ na wana ari mpya ya kurudisha heshima yao kwa mashabiki wao huku akisema kuteleza siyo kuanguka, kwani yalitokea hivi karibuni ndani ya klabu hiyo yamepita na sasa wanakuja kivingine.

“Ukiangalia mechi zilizopita tulipata mabao mawili tu, na raha ya mpira wa sasa ni kufunga mabao mengi, hivyo nimeona ushambuliaji ni tatizo kubwa, lakini tunaendelea na maboresho katika safu hii,” alisema Mwambusi. Asante kwa kutembelea blog hii ya Jambo Tz, ili kuboresha blog yetu tunatoa fulsa ya kutangaza matangazo mbalimbali na pia kutoa maoni yako kupitia namba ya simu (WhatsApp & SMS) 0715 221198, E-mail jambotz8@gmail.com. Merry Chistmass & Happy New Year.

Mwambusi pia alipinga vikali hoja inayotolewa na mashabiki na wadau mbalimbali kwamba Mbeya City ni timu kubwa katika Ligi Kuu.

“Mbeya City bado ni timu changa kwenye ligi, hivyo hata wale wanaoihukumu kwa kufanya vibaya wanakosea ila wanapaswa kuwa na subira kwanza, ndiyo kwanza tuna mwaka mmoja tu kwenye ligi hii hivyo bado ni changa sana, wakubwa na wakongwe ni kama vile Mtibwa Sugar, ambayo ina zaidi ya miaka 10 katika ligi, na sisi laiti tungekuwa na miaka walau minne katika ligi tulipaswa kuhukumiwa, lakini siyo kama ambavyo wanatuhukumu.”

Kuhusu usajili alioufanya katika dirisha dogo Mwambusi alisema haumaanishi kwamba kikosi cha awali kilikuwa kibaya ila ni maboresho madogo dogo na kuimarisha zaidi kikosi chake. Asante kwa kutembelea blog hii ya Jambo Tz, ili kuboresha blog yetu tunatoa fulsa ya kutangaza matangazo mbalimbali na pia kutoa maoni yako kupitia namba ya simu (WhatsApp & SMS) 0715 221198, E-mail jambotz8@gmail.com. Merry Chistmass & Happy New Year.

Na Mwananchi

No comments:

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...