Wednesday, March 28, 2018

JESUS AWAFUTA MACHOZI BRAZIL

Timu ya taifa ya Ujerumani walishindwa kwa mara ya kwanza katika mechi 23 baada ya mshambuliaji wa Manchester City Gabriel Jesus kuwafungia Brazil bao moja na kuwapa ushindi wa 1-0 jijini Berlin.

Hiyo ilikuwa mara ya kwanza kwa mataifa hayo mawili kukutana uwanjani tangu Ujerumani walipowaaibisha Brazil 7-1 katika nusu fainali ya Kombe la Dunia mwaka 2014 mjini Belo Horizonte.
Jesus aliwaweka Brazil mbele kwa mpira wa kichwa dakika za mwishi mwisho kipindi cha kwanza, dakika ya 37.

Alikuwa amepoteza nafasi nyingine ya kufunga muda mfupi awali na kipindi cha pili alipoteza nafasi nyingine pia ambapo aliumpiga mpira nje kwa kichwa lango likiwa wazi baada ya Trapp kutokea kujaribu kuudaka mpira kona ilipopigwa.

Mjerumani Julian Draxler apia alipoteza nafasi ya kufunga mechi ikikaribia kumalizika.

Hii ilikuwa mara ya kwanza kwa Ujerumani ambao ni mabingwa watetezi wa Kombe la Dunia na walioorodheshwa nambari moja duniani kushindwa tangu walipolazwa na Ufaransa nusufainali EURO 2016.

Tangu wakati huo, vijana hao wa Joachim Low walikuwa wameshinda mechi 16 na kutoka sare mechi sita kabla ya mechi hiyo iliyochezewa uwanja wa Olympiastadion.

Ingawa ilikuwa mechi ya kirafiki, ushindi huo ni wa maana sana kwa Brazil ambao wameandamwa na kushindwa kwao Kombe la Dunia miaka minne iliyopita nchini mwao.

No comments:

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...