Saturday, May 17, 2014

USALAMA WA NIGERIA KUANGAZIWA UFARANSA

Kiongozi wa kundi la Boko Haram Abubakr Shekau
Rais wa Ufaransa Francois Hollande anaanda mkutano hii leo mjini Paris kuangazia hali ya usalama nchini Nigeria.
Mkutano huo utawaleta pamoja viongozi kutoka nchi za Nigeria,Benin,Cameroon,Chad na Niger ili kutafuta njia za kukabiliana na kundi la wanamgambo wa kiislamu wa Boko haram.

Wawakilishi wa Marekani muungano wa Ulaya na Uingereza wataangazia kazi iliofanywa na wataalam wa Uingereza, Ufaransa na Marekani waliotumwa nchini humo ili kuisaidia mamlaka ya Nigeria kuwanusuru zaidi ya wasichana 200 waliotekwanyara na kundi hilo. Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz

Chanzo: BBC Swahili

No comments:

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...