Saturday, May 24, 2014

CECAFA NILE BASIN CUP, MBEYA CITY FC KUTUPA KARATA YAO YA KWANZA LEO

IMG_1150 
Na Baraka Mpenja, Dar es salaam WAWAKILISHI wa Tanzania katika michuano mipya ya CECAFA Nile Basin Cup inayoendelea nchini Sudan , Mbeya City fc wanaanza kutupa karata yao ya kwanza leo hii majira ya 11:30 jioni kwa saa za Sudan dhidi ya Academie Tchite ya Burundi. Kuelekea katika mechi hii itakayopigwa uwanja wa Al-Merreikh mjini Khartoum, ushinidi ni muhimu kwa Mbeya City fc ili kupata morali ya mashindano haya yaliyoanza jana kwa mechi tatu kupigwa viwanja viwili tofauti. Kocha Juma Mwabusi ameuambia mtandao huu kwa njia ya simu kutoka nchini Sudan kuwa kikosi chake kipo salama na kipo tayari kwa ajili ya mechi ya leo jioni. “Tumewasili salama mjini Khartoum. Tulichelewa kufika huku ili angalau kuzoa hali ya hewa. Lakini haimaanishi hatuwezi kushindana. Sisi tumejiandaa vizuri na tulikaa Dar kwenye joto ingawa hailingani na Sudan”. “Mashabiki wetu wawe na imani na timu yao. Tunaiwakilisha nchi na tutapambana kwa nguvu zote. Wachezaji wana morali ya kufanya vizuri”. Alisema Mwambusi. Mbali na mchezo huo wa jioni, mechi nyingine ya usiku itakuwa baina ya AFC Leopard ya Kenya dhidi ya Enticelles ya Rwanda. Katika mechi zilizopigwa jana, kwa mujibu wa msemaji wa CECAFA Rodgers Mulindwa, Victoria University ya Kenya iliilaza Malakia FC ya Sudan kusini bao 1-0. Wenyeji Al-Merreikh waliibuka na ushindi mnono wa mabao 3-0 dhidi ya Polisi ya visiwani Zanzibar. Nao Al-Shandi waliibuka na ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Dkhill ya Djibouti. Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz

No comments:

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...