Friday, September 26, 2014

AZAM YAZIPIGA BAO SIMBA NA YANGA


Klabu ya Azam FC ndiyo inayoongoza kwa kulipa posho kubwa wachezaji wake kati ya timu zote 14 zinazoshiriki Ligi Kuu Tanzania Bara.

Uchunguzi uliofanywa na gazeti hili umebaini kuwa wachezaji wa Azam ndiyo vinara wa kupata posho zilizoshiba wakizizidi Yanga na Simba ambao kwa kauli yao wamekubali matokeo.

Mgawanyo huo unaonyesha kwamba Azam kila inaposhinda mechi moja ya ligi inavuna kiasi cha Sh 4milioni, ambapo kila mchezaji anapewa Sh130,000 kiwango ambacho ni kikubwa kwa Simba na Yanga

Kitu kibaya kwa Azam ni pale inapotoa sare au kufungwa, ambapo hakuna chochote watakaochopata ingawa Simba na Yanga huambulia kitu zikitoka sare.

Hata hivyo, kiutaratibu unaonekana utaratibu unaotumiwa na Simba ndiyo mzuri kwani wachezaji wake hupata 40 % ya pato la mlangoni endapo timu hiyo inaibuka na ushindi huku ikiambulia 20% inapopata sare katika michezo yao.

Yanga, ambayo hivi karibuni wachezaji wake waliwasilisha maombi maalumu juu ya kutaka kubadilishiwa viwango vya posho, mpaka sasa wanaambulia kiasi cha Sh70,000 kila mchezaji kwa mechi wanayoshinda na hupata Sh 30,000 wanapopata sare.

“Hatuwezi kushindana na Azam, unajua Azam hata kama haupo katika orodha ya wachezaji wanaocheza mechi, Sh130,000 ipo palepale, lakini Simba na Yanga haipo hivyo, mchezaji anayecheza mechi anapata zaidi ya yule aliyekosa mechi,” alisema mmoja wa mabosi wa Simba ambaye hakutaka jina lake litajwe gazetini. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

No comments:

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...