Friday, February 22, 2013

LOWASSA ATOA OMBI KWA RAIS KIKWETE



Waziri mkuu aliejiuzulu Mh. Edward Lowassa, amemtaka rais Kikwete aunde tume kuchunguza kilichopelekea matokeo mabaya ya form IV mwaka huu. Amesema tume itasaidia kubaini ni nini chanzo cha tatizo.

Wakati huo huo Mh. Lowassa amemsifu kijana aliyemchora Messi na kusema kijana huyo ni intelligent. Amesifu uwezo wa kijana huyo kufanya hivyo!


Vilevile Mh. Lowassa, ameitaka serikali kuongeza uwekezaji katika elimu kwani amesema tofauti na nchi nyingine za Afrika Mashariki, Tanzania ndio ya mwisho kwa uwekezaji kwani inawekeza asilimia moja point something ya GDP katika elimu wakati Kenya ni asilimia tano na Rwanda kama sikosei amesema inawekeza mpaka asilimia 7 ya GDP katika elimu na hivyo ametoa wito kwa serikali kuongeza uwekezaji katika elimu.


Mh. Lowassa pia amemsifu Rais Kikwete kwa kufanikiwa katika maeneo mengine kama ujenzi wa barabara, hospitali, zahanati na kwenye maeneo mengine na kumtaka ajielekeze zaidi katika elimu. Mh. Lowassa amerudia kauli yake na kusisitiza kuwa msimamo wake utabaki kuwa ni elimu kwanza na sio kitu kingine.


Miongoni mwa viongozi waliohojiwa ni pamoja na Zitto Kabwe ambaye mbali na kushauri mambo mbalimbali pia amewataka waziri wa elimu na naibu wake pamoja na katibu mkuu wa wizara ya elimu kujiuzulu.


Source: Clouds FM mchana wa leo/jamiiforum

No comments:

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...