Friday, February 22, 2013

MONTAGE CHARITY BALL KUFANYIKA LEO NDANI YA SERENA HOTELI

 Mkurugenzi wa Kampuni ya Montage Limited Teddy Mapunda akiongea na waandishi wa habari leo katika hoteli ya Serena iliyopo jijini Dar Es Salaam
Teddy Mapunda Akifafanunua Jambo Mbele ya Waandishi wa Habari (hawapo Picha) leo katika Mkutano na waandishi wa habari uliofanyika katika hoteli ya Serena Kulia ni Msanii kutoka Nchini Kenya Kidumu atakaye fanya makamuzi pamoja na Peter Msechu na Barnaba
Mkurugenzi wa Kampuni ya Montage Limited Teddy Mapunda(katikati) Akiteta Jambo Na Msanii Kutoka Nchini Kenya Kidumu (kulia) wakati wa Mkutano na Wahandishi wa Habari uliofanyika katika Hoteli ya Serena Leo na Kushoto ni Msanii wa Bongo Fleva Peter Msechu
Mkurugenzi wa Montage Limited Teddy Mapunda akiongea na Waandishi wa habari (hawapo Pichani) wakati akiongelea Juu ya Tafrija ya Hisani ijulikanayo Kama Montage Charity Ball itakayofanyika Leo katika Hoteli ya Serena Kulia Kwa Teddy Mapunda Ni Peter Msechu na Kutoka Kushoto ni Msanii Barnaba na Kidumu kutoka Nchini Kenya
Pichani ni baadhi ya Wasanii  watakao tumbuiza kwenye tafrija ya Montage Charity Ball itakayofanyika jioni ya leo ndani ya Serena Hotel,jijini Dar.Kutoka kushoto ni Peter Msechu,Kidumu kutoka Kenya,Barnaba pamoja na Deo Mwanambilimbi ambaye ni kiongozi wa Kulunde Band.
Pichani shoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Montage,Teddy Mapunda (katikati) akizungumza na Waandishi wa habari (hawapo pichani) wakati akielezea kufanyika kwa tafrija maalum ya harambee ya kuchangisha fedha kwa ajili ya kusaidia wanawake wenye matatizo ya afya hapa nchini kupitia mfuko wa Montage Charity Ball,itakayofanyika jioni ya leo, Februari 22 kwenye Hoteli ya Serena,jijini Dar es Salaam

Aidha Teddy ameeleza kuwa malengo hasa ni kukusanya kiasi cha zaidi ya shilingi milioni 100 kwa ajili ya kusaidia matibabu ya Wanawake wenye matatizo mbali mbali.Mgeni rasmi katika Tafrija hiyo anatarajiwa kuwa Mwenyekiti wa Taasisi ya Wanawake na Maendeleo (WAMA),Mke wa Rais Mama Salma Kikwete.Kulia kwake ni baadhi ya Wasanii watakaotumbuiza kwenye tafrija hiyo ambao ni Kidumu kutoka Kenya,Barnaba pamoja na Deo Mwanambilimbi ambaye ni kiongozi wa Kulunde Band na Peter Msechu ambaye hayupo pichani.

No comments:

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...