Wednesday, February 19, 2014

TAHADHARI YA MVUA KUBWA FEB 19-21/2014

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA UCHUKUZI
MAMLAKA YA HALI YA HEWA TANZANIA
Simu: 255 22 2460735/2460706

FAKSI: 255 22 2460735/2460700 S.L.P. 3056
Barua pepe: met@meteo.go.tz DAR ES SALAAM
Tovuti:  www.meteo.go.tz
Unapojibu tafadhali nakili:
Kumb. Na.: TMA/1622 18 Februari, 2014

TAARIFA KWA UMMA: VIPINDI VYA MVUA KUBWA VINATARAJIWA.
Taarifa Na. 201402-03
Muda wa Kutolewa
Saa za Afrika Mashariki
Saa 8:30 Mchana

Daraja la Taarifa:- Tahadhari
Kuanzia: Tarehe 19  Februari, 2014 

Mpaka: Tarehe 21 Februari, 2014
Aina ya Tukio Linalotarajiwa ni vipindi vya mvua kubwa (zaidi ya mm 50 ndani ya saa 24) kwa siku.

Kiwango cha uhakika:- Wastani (60%)
Maeneo yanayotarajiwa kuathirika ni Kanda ya kati (mikoa ya Singida na Dodoma), nyanda za juu kusini magharibi (mikoa ya Iringa, Mbeya na Njombe) na maeneo ya kusini  (Mikoa ya Ruvuma na Morogoro).

Maelezo:-
Hali hii inatokana na kuimarika kwa mfumo wa mgandamizo mdogo 
wa hewa katika rasi ya Msumbiji. Mfumo huu unatarajiwa kuvuta 
upepo kutoka misitu ya Congo kupitia maeneo tajwa hapo juu.

Angalizo:-
Idara zinazohusika na hali ya tahadhari pamoja na wakazi wa maeneo 
hatarishi wanashauriwa kuchukua tahadhari.

Maelezo ya Ziada:-
Mamlaka ya Hali ya Hewa inaendelea kufuatilia hali hii na itatoa 
mrejeo kila itakapobidi.

Imetolewa na 
Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania.

Monica Mutoni
Public Relation Office
Tanzania Meteorological Agency

No comments:

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...