Thursday, May 25, 2017

RAIS WA FIFA AIPONGEZA YANGA KWA KUSHINDA UBINGWA WA VPL 2016/2017

Rais wa Shirikisho la Soka Duniani (FIFA), Gianni Infantino ametuma salamu za pongezi kwa uongozi, wachezaji na mashabiki klabu ya Yanga kwa kuibuka washindi wa Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) msimu wa 2016/2017.

Salamu za Infantino zimetumwa kwa Yanga kupitia Rais wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Jamal Malinzi na kuwa pamoja na kuwapongeza kwa ushindi walioupata pia anaitakia kila la kheri Yanga katika michuano iliyopo mbele yake.

No comments:

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...