Wednesday, April 17, 2013

MAKAMBA ASHITAKIWA KWA KINANA

WanaCCM wa Ifakara mjini ‘wamemshtaki’ Katibu Mkuu wa zamani wa CCM, Yusuph Makamba kwa Katibu Mkuu wa sasa wa chama hicho, Abdulrahman Kinana kwa ahadi yake aliyoitoa 2008 ya kuwapatia Sh1 milioni ambayo hajaitimiza. 

Mwenyekiti wa CCM wa tawi la Ifakara mjini, Felista Chakachaka alisema kwamba mwaka 2008, Makamba alipotembelea tawi hilo, aliwaahidi kuwapatia
Sh1 milioni kwa ajili ya kazi za tawi hilo lakini hakuitekeleza.

Hata hivyo, Makamba aliyeko Bumbuli mkoani Tanga, alisema jana: “Sawa, mimi nilitoa ahadi hiyo, sikuitekeleza, sasa aliyepo si ndiyo anatoa...kwani ahadi za Mwalimu Nyerere si Mzee Ali Hassan Mwinyi kazitekeleza, sawa na ahadi za Benjamini Mkapa ambazo Rais Jakaya Kikwete anatekeleza.

“Huyu wa sasa aliyepo madarakani ndiye chama, ile ni ahadi ya chama, ulifikiri Makamba n’toe fedha yangu mfukoni, ile ni ahadi ya chama,” alisema Makamba.

Akijibu hoja hiyo, Kinana alisema kwa kuwa Makamba aliahidi kiasi hicho cha fedha akiwa katibu mkuu, basi yeye atatoa fedha hizo. “Katika kipindi cha wiki mbili fedha hizo zitakuwa zimeingia katika akaunti yenu..nitawapatia kama alivyoahidi alisema Kinana.
Mbali na kutembelea tawi hilo, Kinana alifungua mashina ya wakereketwa matano mjini Ifakara.Kinana yuko ziarani mkoani humo kuangalia maendeleo ya chama hicho tawala.

SOURCE::MWANANCHI:

No comments:

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...