Saturday, June 17, 2017

MANGULA AWATAKA WAPINZANI KUACHA KUDANDIA TRENI KWA MBELE SAKATA LA MCHANGA WA MADINI

Makamu Mwenyekiti wa CCM, Tanzania Bara, Philip Mangula amesema kitendo alichokifanya Rais John Magufuli cha kuwafichua wanaotorosha mchanga wa madini kipo kwenye ilani ya chama hicho hivyo wapinzani waache kudandia treni kwa mbele.

Mangula amesema hayo leo (Jumamosi) wakati akizungumza na wanachama wa CCM kwenye kongamano la kuunga mkono juhudi za Rais na kumpongeza kwa kuwafichua mafisadi lililoandaliwa na wanachama hao.

"Alichokifanya Rais kipo ndani ya ilani ya chama, wapo wanaotaka kudandia treni kwa mbele wakidai wao ndiyo walikuwa na mawazo hayo, nataka niwaambie Rais anatekeleza ilani hiyo ni mipanngo ya CCM, "amesema.

Pia, Mangula amewaonya watu wanaoibuka na kutaka kukwamisha kazi anayofanya Magufuli kuwa hawataweza na nchi haitashtakiwa kama wanavyodai.

“Niwatoe hofu wananchi na wanachama wote kuwa nchi iko salama zaidi tumuunge mkono Rais wetu kuwafichua wezi wa mali za nchi, "amesema

No comments:

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...