Thursday, August 29, 2013

BAADA YA KIMYA KIREFU, GK AIBUKA NA NGOMA MPYA

GK (katikati) akiwa na DJ Fetty (kushoto) na msanii Pauline Zongo (kulia) ndani ya Studio za Clouds FM  
 GK akiwa ndani ya Studio za Clouds FM wakati akielezea kuhusu ujio wake.
MSANII mahiri katika anga za muziki wa Bongofleva, Gwamaka Kaihura 'King Crazy GK' leo ameibuka na singo yake mpya iitwayo Baraka au Laana aliyomshirikisha msanii Yuzo. aka sita baada ya kuwa busy na masomo kitendo kilichopelekea kuupa kisogo muziki kwa muda na kuwafanya mashabiki wake kum-mis katika fani hiyo. Memba huyo wa East Coast Team ameachia ngoma yake mpya leo na anataraji kuachia video yake siku ya Ijumaa Agosti 30, mwaka huu. 
GK alisema kuwa amerudi kwenye game kwa nguvu zote na amewashukuru baadhi ya wadau kama Eric Shigongo, Ruge Mutahaba na Joseph Kusaga kwa kumtia hamasa ya kurudi kwa nguvu mpya baada ya kupotea kwa muda.

No comments:

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...