Thursday, September 26, 2013

PAPA BENEDICT AKANUSHA KUTOKUWAJIBIKA KWA KASHFA ZA KANISA.

papa_g_2_1b32e.jpg
Papa wa zamani Benedict ameibuka kutoka kwenye ukimya binafsi ndani ya Vatican na kukanusha hadharani kwamba alificha vitendo vya manyanyaso ya kingono kwa watoto na mapadri wa kanisa katoliki.
Katika barua ndefu kwa mtunzi wa vitabu wa Italia asiye na dini na mwanamahesabu (Piergiorgio Odifredi) na kuchapishwa jana Jumanne na gazeti la La Republica , Benedict alikana kutokuwajibika kwa kashfa ya ngono kwa watoto.Lakini amesema kanisa lazima lifanye kila iwezalo kuzuia vitendo kama hivyo kutokea tena.
Makundi ya waathirika wamemshutumu Papa huyo kwa kutokufanya vya kutosha kuzuia manyanyaso hayo, kabla ya kuwa Papa na baada , wakati alipoongoza ofisi ya kanuni ya Kanisa, ambayo ilihusika na kesi za manyanyayaso.

No comments:

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...