Wednesday, June 17, 2015

OPERATION ZA UN ZIFANYIWE MABADILIKO

Baraza la usalama la umoja wa mataifa
Ripoti iliyoandaliwa kwa hisani ya umoja wa mataifa imeelezea kuwa oparesheni za kulinda usalama za shirika hilo zinahitaji kufanyiwa mabadiliko makubwa.
Ripoti hiyo imekusanywa baada ya madai kutolewa hivi karibuni dhidi ya vikosi vya umoja huo vya kulinda amani kwamba baadhi wamekuwa wakiwanyanyasa kingono watoto wadogo.
Miongoni mwa mapendekezo ya ripoti hiyo ni kuwa nchi ambako maafisa husika wanatoka, zisikubaliwe kuchangia tena wanajeshi katika vikosi vya umoja wa mataifa.
Pia ripoti hiyo inasema kuwa wanajeshi waliotajwa kuhusika na uovu huo wanastahili wakabiliwe na sheria, na nchi zao pia zinafaa kushurutishwa kueleza wazi ni hatua zipi za adhabu zilizochukuliwa dhidi yao.
Pendekezo jingine lililotolewa katika ripoti hiyo ni kuwa madai yote ya unyanyasaji wa ngono yanastahili kufanyiwa uchunguzi wa kina kwa chini ya miezi sita.
 Je unahitaji kununua gari kwa bei nafuu, bofya hapa au tuambie unataka gari gani na ya bei gani tukutafutie haraka.

No comments:

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...