Wednesday, June 17, 2015

MAN CITY YATOA MILIONI 35 KUMNUNUA STERLING

Man City yatoa pauni milioni 35m kumnunua Raheem Sterling

Klabu ya Manchester City imeimarisha ombi la kumsajili mashambulizi machachari wa Liverpool Raheem Sterling.
Mabingwa hao wa mwaka wa 2014 wametoa pauni milioni 35 sawa na dola milioni 55 kusajili huduma za mshambulizi huyo.
The Reds walikataa ombi la kwanza la kumsajili kiungo huyo mwenye umri wa miaka 20 wakisema thamani yake ni pauni milioni 50.
Kuwepo kwa mchezaji huyo raia wa Uingereza katika soko kumetokana na nia yake ya kuondoka Liverpool .
Sterling alijiunga na Liverpool mwaka wa 2010 akitokea QPR kwa mkataba utakaomalizika mwaka wa 2017.
Brendan Rodgers anamtarajia Sterling kusalia Anfield hadi kandarasi yake itakapokatika 2017.
Hata hivyo alizua mjadala baada ya kuzima pendekezo la nyongeza ya mshahara wake hadi pauni laki moja kwa wiki.
Manchester City inaaminika kuwa iko tayari kutoa marupurupu mengine yatakayofikisha gharama yake hadi pauni milioni 40 japo wanalalamika kuwa Liverpool imeongeza maradufu thamani yake ikifahamika kuwa wenyewe hawakuwa hata wakimlipa pauni laki moja kwa juma.
Kwa upande wake kocha Brendan Rodgers anashikilia kukutu kuwa anamtarajia Sterling kusalia Anfield hadi kandarasi yake itakapokatika.

No comments:

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...