Monday, March 11, 2013

Tigo yampeleka nchini China Mshindi wa Promosheni ya Ascend Y200 Bw.Christian Mkama.


Mshindi wa droo ya Ascend Y200 ya mwaka jana bw. Christian Evarist Mkama akiongea na waandishi wa habari uwanja wa ndege wa kimataifa JK Nyerere kabla ya safari kuelekea nchini China.
Mshindi wa droo ya Ascend Y200 ya mwaka jana bw. Christian Evarist Mkama akiwa na mama mzazi Bi. Eva Christian Amuko na mjomba wake bw. Fortunatus Christian Amuko uwanja wa ndege JK Nyerere kabla ya safari kuelekea nchini China.
Tigo Tanzania imempeleka Bw. Christian Evarist Mkama nchini China ambaye ni mmoja kati ya washindi wawili wa droo ya kwanza ya Ascend Y200 ambayo ilifanyika mwaka jana tarehe 19 Desemba.
 
Kwa kuwa mshindi wa droo hii amejishindia tiketi ya bure ya kwenda na kurudi nchini China pamoja na kulipiwa gharama zote za safari,chakula na dola 200 kwa siku za matumizi.
 
Akiwa nchini china mshindi huyu atakaa siku nne na atatembezwa na kuonyeshwa sehemu mbalimbali za mji wa Guangzhou, na kupelekwa kwenye sehemu za utalii ya mlima Lotus.
 
Promosheni ya AscendY200 ilizinduliwa mwaka jana 2012 mwezi wa kumi(oktoba) kwa jumla kutakuwa na droo tano za Ascend Y200 na kila droo itakuwa na washindi wawili kwa jumla ya washindi kumi watapatikana kwenye droo hizi.
 
Kushiriki kwenye shindano hili mteja wa Tigo inambidi awe amenunua simu ya Ascend Y200 kwenye maduka ya Tigo yaliyosajiliwa na kujisajili kwenye kifurushi cha A-Smart package.

No comments:

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...