Monday, March 11, 2013

WANANCHI WA MOROGORO WAMPONGEZA PADRE RICARDOMARIA

Padre Ricardo Maria ambaye anamiliki shule mbili za sekondari mkoani morogoro nilimnasa juzi kati pande za Mji mpya mkoani hapa akielekea kwenye moja wa shule zake zilipo maeneoe ya Nane Nane akitumia usafiri wake wa baiskeli.

Habari kutoka ndani ya shule hizo za raia huyo wa ltalia zinadai kwamba mtumishi huyo wa mungu asiye vaa viatu kutokana na imani ya dhehebu lake,hupokea watoto yatima na kuwasomesha bure kwenye shule zake. 

Mungu akubariki sana mtumishi wa mungu usiyekuwa na makuu licha ya kujaliwa kuwa na kipato kizuri ikumbukwe pia Padre huyu ni mmoja wa wakurugenzi wa Radio Ukweli inayomilikiwa na kanisa katoriki jimbo la Morogoro.[PICHA NA DUSTAN SHEKIDELE,MOROGORO]

No comments:

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...