Friday, October 17, 2014

DIDA, JAJA, WABEBA JUKUMU ZITO YANGA


kipa Deogratius Munishi 'Dida' 

Pambano la watani wa jadi, Yanga na Simba kesho kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam litakuwa mtihani mkubwa kwa nyota watatu wa Yanga kwa sababu tofauti.

Watatu hao ni mshambuliaji, Genilson Santos ‘Jaja’ , kipa Deogratius Munishi ‘Dida’ na kiungo Andrey Coutinho.

Jaja, aliyeibuka shujaa ghafla alipoitungua Azam kwa mabao mawili kwenye mchezo wa Ngao ya Jamii, kisha akapoteza makali tangu Ligi Kuu ianze,  ana deni kubwa kwa mashabiki wenye matumaini kwake kuwa atafungua akaunti ya mabao dhidi ya Simba.

Makali yake ya Septemba 14 alipoisulubu Azam yaliyomkatia tiketi ya kuwa kipenzi cha mashabiki na  yanaweza kuongezeka au kufutika.

Mbrazili huyo kipenzi cha mashabiki wa Yanga, ingawa pia anaweza kuwa na wakati mgumu kesho kuthibitisha uwezo wake, kutetea nafasi yake kwenye kikosi  cha kwanza, akishindwa kuisaidia Yanga kuchomoza na ushindi, itakuwa tiketi yake ya kusahaulika. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Dida na rekodi za Kaseja, Barthez

Msimu uliopita, kipindi kama hiki, Mustapha Ali ‘Barthez’ alikuwa kipa nambari moja, akisaidiana na Dida, lakini baada ya mchezo wa watani uliomalizika kwa sare ya mabao 3-3, aligeuka adui kwa mashabiki.

Kipa huyo alipotea kwenye ramani ya klabu hiyo, akikosa namba kwenye kikosi hicho, nafasi yake ilichukuliwa na mkongwe, Juma Kaseja  aliyekuwa amesajiliwa.

Kaseja, au ‘Tanzania One’ kwa miaka mingi hakutamba kwani kibarua chake cha kwanza kabla ya mzunguko wa pili wa ligi kuanza, kilikuwa ni mechi  dhidi ya Simba kwenye mchezo wa Nani Mtani Jembe aliporuhusu mabao rahisi na Yanga kufungwa 3-1.

Ndipo Kaseja alipoingia kwenye matatizo baada kujaribu kumpiga chenga Awadh Juma, alishindwa na kusababisha bao la tatu, huo ukawa mwisho wake na mwanzo wa  kuwekwa benchi na nafasi yake kukabidhiwa kwa Dida,  ambaye ujio wa Kaseja ulionekana kumtupa kwenye chaguo la tatu.

Hivyo, mtihani  kwa Dida ni kulinda vyema lango la Yanga kwa umakini, kusahau masaibu ya watangulizi  wake, walioponzwa na matokeo ya mechi dhidi ya Simba.

Ni kawaida, Yanga inaposhindwa kutamba kwa Simba, kipa mmoja  huonja benchi au kutimuliwa.
Kwa staili hiyo, Dida akishindwa kufanya makubwa kwenye mchezo wa kesho, anaweza kuishia benchi na nafasi yake kuchukuliwa na Kaseja au Barthez.
Naye Coutinho, aliyefunga bao la mkwaju wa adhabu ndogo dhidi ya Prisons katika ushindi wa mabao 2-1 wa Ligi Kuu, amekuwa hafanyi mambo makubwa kulinganishwa na mategemeo ya mashabiki. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz
Hilo, linamweka kwenye mtihani dhidi ya Simba, ambayo imesheheni kwenye kiungo, ingawa ukuta una nyufa.
Mtoto kipa Yanga kuidakia Simba
Kuumia kwa wazoefu, Ivo Mapunda na Hussein Shariff kuinaifanya Simba ibaki na kipa mmoja mwenye uhakika wa asilimia 100 kucheza kesho. Huyo  ni mtoto wa kipa wa zamani wa Yanga, Peter Manyika.
Manyika Peter alijiunga Simba kabla ya msimu huu na hajadaka mechi yoyote ya ligi, lakini anategemewa kulibeba jukumu hilo zito. Huo ni mtihani wake wa kwanza ambao utamvusha au kumwangusha kinda huyo.
Vikosi vinatarajiwa kuwa:
Kocha Marcio Maximo anaweza kuwapanga; Deogratius Munishi ‘Dida’, Juma Abdul, Oscar Joshua, Said Makapu, Rajabu Zahir, Mbuyu Twite, Simon Msuva, Hassan Dilunga,  Genilson Santos ‘Jaja’, Haruna Niyonzima na Andrey Coutinho.
Mabeki chipukizi, Said Makapu na Rajabu Zahir wanaweza kurithi  nafasi za wakongwe, Kevin Yondani na Nadir Haroub ‘Cannavaro’ wanaosumbuliwa na majeraha.
Kikosi cha Simba iliyokuwa Afrika Kusini kinaweza kuwa: Manyika Peter, William Lucian, Mohamed Hussein ‘Tshabalala’, Joseph Owino, Hassan Isihaka, Jonas Mkude, Ramadhani Singano ‘Messi’, Shaaban Kisiga, Amissi Tambwe, Emmanuel Okwi, Haroun Chanongo. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

No comments:

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...