Saturday, October 18, 2014

RIPOTI MAALUM: WAFUNGWA WAENDESHA UHALIFU GEREZANI


Pingu za wahalifu

Wakati Serikali ikihaha kukabiliana na vitendo vya uhalifu, imebainika kuwapo kwa mtandao wa uhalifu ambao unawawezesha baadhi ya watu waliofungwa kuratibu matukio ya uhalifu wakiwa gerezani katika mikoa ya Kanda ya Ziwa.

Uchunguzi wa gazeti hili katika eneo hilo uliojumuisha Mikoa ya Mwanza, Simiyu, Geita, Shinyanga, Mara na Kigoma, umebaini kuwa uhalifu huo unahusisha ujambazi, mauaji ya kukodiwa na ujangili wa wanyamapori na watuhumiwa wanatajwa kuwa ni baadhi ya wafanyabiashara na wanasiasa.

Kutokana na nguvu uliyonayo, mtandao huo umekuwa ukitekeleza vitendo vya uhalifu kwa kufanya mawasiliano na watu wao waliofungwa kifungoni kwa kutumia askari na watendaji wengine wa Serikali wasio waaminifu.

Kwa nyakati tofauti watendaji wakuu wa polisi na magereza katika mikoa hiyo, wamezungumzia hali hiyo na baadhi wakionyesha kukiri kwa kueleza; ‘uhalifu wowote lazima uwe na mtandao na kwamba mtu yeyote anaweza kuwa mhalifu.’ Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

“Wafungwa kuendesha uhalifu inawezekana. Inaweza kusababishwa na aina ya rushwa, wapo wafungwa wenye akili pengine zaidi ya askari, wakaweza kuwashawishi pia wanawatumia,” alisema Mkuu wa Gereza Kuu la Butimba mkoani Mwanza,

Jail Mwamgunda. Katika mahojiano maalumu ofisini kwake hivi karibuni Mwamgunda alisema: “Utandawazi unachangia hayo, wakati sheria nyingi zimepitwa na wakati na vitendea kazi bado siyo vya kutosha.

Yapo mawasiliano, zamani ilikuwa barua, sasa simu za mkononi, televisheni ni vigumu kuvidhibiti. Shida hasa ipo kwa wafungwa na mahabusu wanaotoka kwenda nje ya magereza na kurejea kama wana kesi nyingine.

Pia, kuna shida ya uadilifu kwa baadhi ya watendaji. Hata hivyo, sisi Magereza tupo makini, askari akipatikana na kosa la aina hiyo, sheria iko wazi anafukuzwa kazi.”

Uchunguzi huo uliohusisha wananchi wa kawaida na watendaji wa kada mbalimbali ikiwamo wa Jeshi la Polisi, Magereza na Mamlaka ya Hifadhi za Taifa (Tanapa) katika maeneo tofauti ya mikoa hiyo, umethibitisha kuwapo kwa matukio hayo.

Rushwa, tamaa ya utajiri, kipato hafifu, kukosa uaminifu pia ushirikiano miongoni mwa watendaji wa Serikali ikiwamo wanasheria, waendesha mashitaka, polisi na magereza na kukua kwa utandawazi vinatajwa kuwa miongoni mwa sababu za kukithiri uhalifu huo katika mikoa hiyo.

Katika hali isiyo ya kawaida baadhi ya watuhumiwa hao walio mahabusu na katika magereza kwenye ukanda huo huwasiliana na mtandao wao wa uhalifu ulio nje kwa barua, simu na njia nyingine.

Wahalifu hao kutumia mtandao wao ikiwamo jamaa zao wanaowaagiza kupeleka rushwa kwa baadhi ya wasimamizi wa sheria ili kufanikisha mikakati yao ya kutoka, kubadilishiwa mashtaka au kukata rufaa zitakazowawezesha kupata dhamana na kuweka mkakati maalumu wa kutoka gerezani.

Habari hizo zinapasha kuwa licha ya baadhi ya watuhumiwa kukamatwa kwa uhalifu wa kukutwa na silaha, mauaji hata ujangili na Kikosi Maalumu cha Shirika la Hifadhi za Taifa (Tanapa) na askari polisi katika kukabili wimbi hilo, baadhi ya wahusika ya hawajawahi kusomewa mashtaka.
Hali hii mbaya zaidi katika mikoa yenye hifadhi za taifa za wanyamapori ambako licha ya uhalifu, walinzi na watendaji wengine wa maeneo hayo wanaishi kwa hofu kutokana na kutishiwa maisha na wahalifu wanaowakamata na wengine wakieleza kunusurika kifo mara kadhaa kutokana na kushambuliwa na wahalifu wanaoingia hifadhini. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz
Itaendelea Kesho

Na Mwananchi

No comments:

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...