Monday, October 13, 2014

MSOMI MKENYA PROFESA MAZURI AFARIKI

Profesa Mazuri alisifika sana kwa kuangazia tamaduni za kifarika kwa dunia nzima
Msomi mashuhuri wa Kenya,duniani Profesa Ali Mazrui ameaga dunia nchini Marekani.
Mazrui alikuwa msomi wa maswala ya kisiasa, utamaduni wa kiafrika na maswala ya dini ya kiisilamu.
Mazrui aliyekuwa na umri wa miaka 81 alifariki nchini Marekani ambako amaekuwa akiishi baada ya kuugua kwa mda mrefu.
Duru zinasema kuwa Profesa Mazrui atazikwa mjini Mombasa Pwani ya Kenya alikozaliwa.
Alitoa ombi la kutaka kusikwa Mombasa kabla ya kifo chake akisema angependa kuzikwa katika jumba la kihistoria la Fort Jesus.
Kabla ya kifo chake Marehemu Mazrui alikuwa anafunza katika chuo kikuu cha Binghamton mjini New York. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

No comments:

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...