Friday, March 08, 2013

IPO HAJA YA KUJIFUNZA KUTOKA FINLAND- MASELE

1 69aac
Naibu Waziri wa Nishati na Madini anayeshughulikia masuala ya madini, Mhe. Stephen Masele, akimuonesha Balozi wa Finland nchini,Sinikka Antila ramani ya maeneo ambapo kuna madini na uchimbaji unaendelea.
Serikali imesema inahitaji kujifunza zaidi kutoka Finland hususan katika uchimbaji wa madini ili kuwa na uchimbaji wenye tija kwa taifa.Hayo yalisemwa na Naibu Waziri wa Wizara ya Nishati na Madini, Stephen Masele alipokutana na Balozi wa Finland nchini, Sinikka Antila.Masele alisema Tanzania inahitaji kujifunza masuala ya uchimbaji madini kutoka Finland kwa kuwa mazingira ya uwekezaji ya nchini humo yanashabihiana na mazingira ya uwekezaji nchini Tanzania.“Unajua kampuni kubwa zinazojishughulisha na uchimbaji madini nchini Finland siyo za hapo Finland bali ni kampuni kutoka nchi nyingine yani multi-nationals na hili pia ndilo linalofanyika hapa kwetu Tanzania” alisema.

No comments:

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...