Friday, March 08, 2013

Vigogo wavuliwa madaraka TBS


Bodi ya Wakurugenzi ya Shirika la Viwango Tanzania (TBS), imewavua madaraka wakurugenzi wawili.
Mwenyekiti wa Bodi hiyo, Profesa Cuthbert Mhilu alisema jana kuwa waliovuliwa madaraka ni aliyekuwa Mkurugenzi wa Udhibiti Ubora, Dominic Mwakangale na aliyekuwa Mkurugenzi wa Upimaji na Huduma za Vifungashio, Kezia Mbwambo.
Profesa Mhilu alisema hatua hiyo imekuja baada ya bodi hiyo kufanya usaili kwa vigogo mbalimbali wa shirika hilo ulioanza juzi asubuhi hadi saa 3:00 usiku.
Katika taarifa hiyo, Profesa Mhilu ambaye hakutaka kuingia kwa ndani juu ya hatua hiyo, alisema viongozi hao watapangiwa kazi nyingine.
“Kwa kipindi kirefu, TBS imekuwa ikikabiliwa na matatizo mbalimbali yaliyochangia kudhoofisha utendaji wa watumishi na kulifanya shirika kukosa tija na ufanisi. Bodi imeonelea ikae mara moja kuchambua, kujadili na hatimaye kufikia uamuzi wenye lengo la kuweka mazingira bora na kuwezesha kuanza utatuzi wa matatizo ili shirika lifikie malengo yake.”

No comments:

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...