Friday, March 08, 2013

HII NDIO TAARIFA YA ALIEUWAWA NA SIMBA AKIWA KWENYE TENDO LA NDOA

.
.
Taarifa kutoka Zimbabwe ni kwamba mwanamke mmoja aitwae Mai Desire amefariki kwa kushambuliwa na Simba aliewakuta yeye na mpenzi wake wakifanya tendo la ndoa kwenye kichaka ndani ya eneo la kijiji karibu na shule ya msingi ya Mahombekombe.
Mashuhuda wanasema wakati mwanamke huyo akishambuliwa na Simba, boyfriend wake alifanikiwa kukimbia akiwa uchi huku akiwa bado amevaa kinga (Condom)
Mwanaume huyo alikimbia  kuomba msaada akiwa mtupu bila nguo lakini wengi hawakumuamini wakijua ana upungufu wa akili.
.
Baadae ndio watu walimuamini na kumsindikiza polisi alikopewa msaada wa polisi na askari wa Wanyama pori Zimbabwe na kuelekea mpaka kwenye eneo la tukio ambako ilifyetuliwa risasi moja na kukuta mwanamke ameshafariki tayari huku akiwa ametapakaa damu mwili mzima na kujeruhiwa vibaya mwilini ikiwemo shingoni ambapo waumini wa kanisa moja karibu na hapo walitoa ushuhuda wa kuona Simba 7 kwenye eneo la tukio.
Wakati huohuo mwili wa mwanaume mmoja ambae hakutambulika kirahisi ulikutwa akiwa ameshafariki karibu na ZESA social club huku My Zimbabwe wakiripoti mwanaume huyo kushambuliwa na Simba muda mfupi uliopita.
Tukio jingine liliripotiwa kwamba mwanaume aitwae Musinje pia alishambuliwa na Simba na kufariki dunia wakati akitoka kwenye club ya usiku ambapo mwili wake ndio uligundulika baadae ambapo Wakazi wa Kariba wanasema ni watu watatu wameuwawa na Simba kwenye eneo hilo ndani ya saa 24.

No comments:

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...