Friday, January 23, 2015

HATIMA YA MUHONGO NDANI YA SAA 48 ZIJAZO...!!!

Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo.

Zikiwa zimebaki siku tatu kabla ya Bunge la Jamhuri ya Muungano kuanza mjini Dodoma, sasa hakuna shaka kwamba Rais Jakaya Kikwete atafanya mabadiliko katika Baraza la Mawaziri wakati wowote kuanzia leo na kabla ya Jumapili (saa 48) kutokana na kukabiliwa na safari ya nje.
Rais anatarajiwa kufanya mabadiliko hayo baada ya kumwondoa Anna Tibaijuka, ambaye alikuwa Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa kuhusishwa na kashfa ya uchotwaji fedha kwenye Akaunti ya Tegeta Escrow baada ya kuingiziwa Sh1.6 bilioni kwenye akaunti yake.
Mwingine ni Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo, ambaye anatuhumiwa kutoshughulikia kwa makini sakata hilo na kusababisha Serikali kupoteza fedha hivyo kuwapo kwa uwezekano mkubwa wa kumvua uwaziri utakaomlazimu Rais kufanya mabadiliko madogo kwenye baraza lake, ikiwa ni miezi isiyozidi mitano kabla ya kuvunja Bunge kupisha Uchaguzi Mkuu wa Oktoba.
Habari ambazo Mwananchi imezipata zinaeleza kuwa Rais Kikwete anaweza kutangaza mabadiliko hayo wakati wowote kuanzia leo. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.
“Rais anaondoka Jumapili kwenda Davos (Uswisi kuhudhuria mkutano wa Jukwaa la Kiuchumi la Dunia (WEF)), hivyo kwa jinsi yoyote ile ni lazima atangaze baraza kesho (leo) au Jumamosi,” alisema mpashaji habari wetu.
“Hawezi kutangaza baraza jipya akiwa nje ya nchi, hivyo ni lazima atangaze kesho (leo) au ikishindikana Jumamosi ili Jumapili afanye shughuli nyingine na kuondoka.”
Hata hivyo, mabadiliko ya mwisho ya Baraza la Mawaziri yalitangazwa na Katibu Mkuu Kiongozi, Ombeni Sefue ambaye pia anaweza kupewa kazi hiyo.
Baada ya kujadili sakata la uchotwaji wa fedha hizo kwa takriban siku nne, Novemba 28, mwaka jana Bunge lilifikia maazimio manane, likiwamo la kutaka wote waliohusika kwenye kashfa hiyo wachukuliwe hatua na mamlaka husika, akiwamo Profesa Muhongo ambaye Rais Kikwete alisema Novemba 22, 2014 kuwa amemuweka kiporo hadi baada ya “siku mbili au tatu” kusubiri matokeo ya uchunguzi.
Hata hivyo, shinikizo liliongezeka baada ya Kamati Kuu ya CCM, iliyokutana Zanzibar chini ya uenyekiti wa Rais Kikwete, kuitaka Serikali iwe imetekeleza kwa vitendo maazimio yote ya Bunge kuhusu sakata hilo kabla ya kikao cha Bunge kitakachoanza Jumanne ijayo na kutaka wahusika walioko kwenye dhamana za uteuzi wachukuliwe hatua stahili na mamlaka zao kuwawajibisha mara moja.
Pia, Kamati ya Maadili ya CCM iliyokutana Dar es Salaam mapema wiki hii, iliwajadili wanachama waliohusika kwenye kashfa hiyo na kupeleka taarifa yake kwenye Kamati Kuu ya chama hicho kwa hatua zaidi.
Wakati CCM ikisema hayo, wabunge wamekuwa wakimkumbusha kiongozi huyo wa Serikali kuchukua hatua kabla ya kikao cha Bunge. Wabunge wawili wa mkoani Arusha, Godbless Lema na Joshua Nassari wote kupitia Chadema, wamediriki kusema kuwa watamwondoa Profesa Muhongo kwa mabavu kwenye ukumbi wa chombo hicho cha kutunga sheria iwapo Rais hatakuwa amemuondoa.
Pia, nchi wahisani zilieleza mapema mwezi huu kuwa pamoja na kuruhusu kiasi cha fedha kwa ajili ya miradi ya maendeleo, bado zinasubiri tamko la Serikali kuhusu sakata hilo, ikiwa ni pamoja na hatua ilizochukua kuzuia kashfa kama hiyo isitokee tena, ili Tanzania inufaike kwa misaada hiyo ya fedha zinazotokana na walipakodi wa nchi zao.
Wapinzani wanamlaumu Rais Kikwete kwa kuchelea kumwondoa Profesa Muhongo baada ya kuahidi mwezi mmoja uliopita kuwa angelifanyia uamuzi suala lake katika muda wa siku mbili au tatu tangu Desemba 22 mwaka jana.
Kuna habari kwamba kuchelewa kutangazwa kwa mabadiliko hayo pengine kunatokana na Rais Kikwete kusubiri ripoti ya uchunguzi wa kashfa ya Operesheni Tokomeza, ambayo habari zinasema inaweza kuwasafisha baadhi ya mawaziri na hivyo kumpa mwanya wa kuwarejesha, hasa kutokana na muda wa uhai wa baraza hilo kuwa mfupi, hivyo angehitaji watu ambao ameshafanya nao kazi.
Kabla ya kutangaza hatua alizochukua kwa mujibu wa maazimio ya Bunge, Rais Kikwete alikatisha ziara ya Waziri Mkuu Mizengo Pinda aliyekuwa Arabuni, kitendo kilichotafsiriwa kuwa alitaka ushauri kuhusu mawaziri waliohusika na hatua za kuchukua, lakini akatangaza kumvua uwaziri Profesa Tibaijuka pekee.
Awali, Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) ilipendekeza kuwa Waziri Pinda naye awajibishwe kutokana na kushindwa kushughulikia suala hilo akiwa mtendaji mkuu wa Serikali.
Aidha, habari ambazo Mwananchi imezipata zinasema kuwa Rais Kikwete pia alitaka kutumia fursa hiyo kuwaondoa mawaziri wote waliotangaza nia ya kugombea urais kutokana na kusakamwa kuwa wanatumia nafasi zao vibaya, huku wakivunja taratibu za CCM.
Hata hivyo, kutokana na ukweli kuwa Pinda ni miongoni mwa waliotangaza nia, itakuwa vigumu kwake kumuondoa mtendaji huyo mkuu kwa kuwa itamaanisha kuvunja Serikali.
Katika sakata la Tegeta Escrow, zaidi ya Sh306 bilioni zilichotwa kwenye akaunti hiyo iliyokuwa Benki Kuu ya Tanzania (BoT) ambayo ilifunguliwa kwa pamoja na Tanesco na kampuni ya IPTL, ambayo iliingia mkataba wa kuliuzia umeme shirika hilo la umma, baada ya pande hizo mbili kuingia kwenye mgogoro wa viwango vya tozo na hivyo kufungua kesi mahakamani.
Kesi hiyo iliisha kwa jaji kuamua kuwa pande hizo mbili zikokotoe upya viwango vya tozo hiyo, lakini fedha zote zilizokuwamo kwenye akaunti hiyo zikaondolewa mwishoni mwa mwaka jana na kulipwa kwa Kampuni ya Pan African Power Solutions (PAP), ambayo ilinunua hisa zote za umiliki wa IPTL.
Wakati malipo hayo yanafanyika, kulikuwa na pingamizi la Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) ambayo ilitaka kodi ambayo Tanesco ilitakiwa ilipe, ikatwe kwanza kabla ya IPTL kulipwa fedha zake, huku ikihoji kodi nyingine katika ununuzi wa hisa za kampuni nyingine iliyomiliki kwa muda hisa za IPTL ya Piperlink ulioonekana kutawaliwa na udanganyifu.
Tayari Jaji Frederick Werema, aliyekuwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali, ameshajiuzulu wadhifa huo, wakati Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, Eliakim Maswi amesimamishwa kazi kupisha uchunguzi. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.
Wenyeviti watatu wa kamati za Bunge, William Ngeleja, Andrew Chenge na Victor Mwambalaswa, wamejiuzulu nyadhifa zao, ikiwa ni sehemu ya maazimio ya Bunge. Pia kuna mlolongo wa viongozi wa umma, vigogo wa zamani wa Serikali na watumishi wa umma walioingiziwa fedha na mmiliki wa zamani wa Kampuni ya IPTL, James Rugemarila ambazo zinahusishwa na kashfa hiyo au kutotangaza masilahi binafsi katika vikao vilivyohusu sakata hilo.
Chenge, aliyewahi kuwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali ambaye ni Mbunge wa Bariadi, aliingiziwa Sh1.6 bilioni, Ngeleja, waziri wa zamani wa Nishati na Madini na Mbunge wa Sengerema aliingiziwa Sh40.4 milioni, wakati Mwambalaswa ameondolewa kutokana na kuwa mwenyekiti wa Kamati ya Nishati na Madini wakati huohuo akiwa mwenyekiti wa Bodi ya Tanesco iliyotuhumiwa kushindwa kushughulikia vizuri sakata hilo.
Wakati hayo yakiendelea, Taasisi ya Kudhibiti na Kupambana na Rushwa (Takukuru) imeshawafikisha mahakamani maofisa sita waandamizi wa TRA, Tanesco na BoT kwa tuhuma za kuhusika kwa njia moja au nyingine kwenye kashfa hiyo.
Kauli ya wasomi
Aliyekuwa Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha St Augustine, Dk Charles Kitima alisema: “Nchi lazima iundwe na Serikali imara na itakayoendeleza mikakati yake ya maendeleo. Tunakwenda katika uchaguzi hivyo nchi inahitaji Serikali yenye viongozi madhubuti.”
Huku akitolea mfano Uchaguzi Mkuu utakaofanyika Oktoba na Kura ya Maoni kupitisha Katiba Mpya, Dk Kitima alisema mambo hayo yanahitaji viongozi makini wa kuyasimamia.
Mhadhiri wa Chuo Kikuu Dar es Salaam, Bashiru Ally alisema: “Nadhani mabadiliko yanaweza kuwa makubwa kutokana na matukio yaliyopo mwaka huu. Yanaweza kuwa ni mabadiliko ya kuhakikisha kuwa Serikali iliyopo madarakani inaendelea kuwapo. Mabadiliko ya kuisaidia CCM kushinda.”
Aliungana na Dk Kitima, kusisitiza kuwa sakata la escrow, Uchaguzi Mkuu na Kura ya Maoni ni kati ya mambo yanayoweza kuchangia kufanyika kwa mabadiliko makubwa. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

Na Mwananchi

No comments:

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...