Sunday, September 07, 2014

HAYA NDIO MAAMUZI YA WAZIRI MWAKYEMBE KUFUATIA AJALI ILIYOTOKEA MUSOMA NA KUUA WATU 39

Waziri wa uchukuzi, Mhe Harrison Mwakyembe
Kufuatia ajali ya mabasi iliyoua takbriban watu 39 Musoma, Waziri wa uchukuzi, Mhe Harrison Mwakyembe amefanya maamuzi kadhaa, kupunguza ajali za barabarani. Ifuatayo ni kauli yake:
1.Tunaanza na hawa waliopata ajali, nimeelekeza na najua vyombo vinavyohusika Polisi pamoja na SUMATRA watatekeleza… kwanza kuzifungia kampuni za haya mabasi ya J4 na Mwanza Coach wasijihusishe na usafirishaji wa abiria tena, hatuwezi kuwa tunapata ajali za kijingajinga namna hiyo, nimeliona eneo lenyewe liko wazi kabisa lakini ni watu tu wameamua, dereva wa huku anamuona mwenzake na kusema mimi lazima anipishe’ – Dr. Mwakyembe
2. Tumeelekeza Wafanye uhakiki wa madereva wao wote na tunahitaji picha zao lakini vilevile tunahitaji mikataba ya kazi, hatutaki mabasi ya kupeleka abiria yaendeshwe na watu tu kwa majaribio, nataka ushahidi wa kila dereva kwamba amejiunga na hii mifuko ya akiba ya Wafanyakazi, tuone kabisa mchango wa Mwajiri na mfanyakazi kila mwezi’
3. Nimeagiza lazima tuangalie BIMA ya hiyo gari, unajifikiria mwenyewe tu ukipoteza gari ulipwe kidogo gari yako lakini hufikirii kuhusu binadamu…. bila comprehensive haendeshi mtu gari kuchukua abiria.
Tamasha la Fiesta lililokua lifanyike Ijumaa hapa Musoma sasa imefahamika litafanyika Jumapili ya kesho September 7 2014 ambapo pia imehamasishwa kwa wingi watu kujitokeza ili mapato hayo yapelekwe kwa ndugu waliopoteza watu na majeruhi ajalini. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

No comments:

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...