Friday, June 26, 2015

BURUNDI KUENDELEA NA RATIBA YA UCHAGUZI

Gervais Rufyikiri aliyekuwa makamu wa rais wa Burundi amekimbilia Ubelgiji. 

Serikali ya Burundi imesema haitashiriki katika mazungumzo yaliyodhaminiwa na Umoja wa Mataifa yakilenga kupunguza hali ya uhasama uliopo kabla ya kufanyika kwa uchaguzi wenye utata.

Waziri wa mambo ya ndani, Edouard Nduwimana, amsema ratiba ya uchaguzi haitabadilika.

Maandamano yamekuwa yakiendelea kwa wiki kadha kupinga hatua ya Rais Pierre Nkurunziza kutaka kuwania nafasi ya urais kwa mara ya tatu.

Viongozi wawili katika serikali ya Rais Nkurunziza - akiwemo mmoja wa makamu wa rais, Gervais Rufyikiri, na spika wa bunge la nchi hiyo, Pie Ntavyohanyuma, wamekimbilia Ubelgiji.

Wote wawili wamekuwa wakosoaji wa rais. Uchaguzi umepangwa kufanyika mwezi uajao. Uchaguzi wa wabunge unafanyika Jumatatu.

No comments:

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...