Tuesday, March 24, 2015

KAVUMBAGU: UWANJA ULITUKWAMISHA TANGA

 

Mabeki wa Coastal Union wakiwahani mpira na wachezaji waAzam wakati wa mchezo wa Ligi kuu Tanzania Bara uliochezwa kwenye uwanja wa Mkwakwani ,Tangajuzi.Azam ilishinda 1-0.

Mshambuliaji wa Azam FC, Didier Kavumbagu amesema walihitaji ushindi wa zaidi ya bao moja dhidi ya Coastal Union ila walikwamishwa na uwanja mbovu wa Mkwakwani na kushindwa kuonyesha kiwango chao cha juu.

Mechi hiyo iliyochezwa juzi ilimalizika kwa ushindi wa bao 1-0 kwa Azam na kuendelea kukaa katika nafasi ya pili kwenye msimamo wa Ligi Kuu Bara ikiwa na pointi 36 nyuma ya pointi moja dhidi ya Yanga wenye 37.

Bao pekee la Azam lilifungwa na mshambuliaji wao, John Bocco, na Kavumbagu alilazimika kutolewa nje huku nafasi yake ikichukuliwa na Gaudence Mwaikimba. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

Kavumbagu aliliambia gazeti hili kuwa anaamini bado ana nafasi ya kufunga zaidi katika mechi zilizobaki lakini kwa sasa anaangalia zaidi ushindi wa timu ili iweze kutetea ubingwa, hivyo mchezaji yeyote atakayeifungia Azam hataweza kuharibu mahesabu yake.

“Hii mechi tungepata mabao mengi ila uwanja umetukwamisha sana, nafurahi timu yangu imeshinda japo kwa ushindi wa bao moja, naamini nitafunga mechi zijazo na ninafurahi mchezaji mwenzangu anapoifungia Azam kwani wote tupo kwa ajili ya kufanikisha tunatetea ubingwa,” alisema Kavumbagu.

Kavumbagu ameshafunga mabao kumi akifuatiwa na Simon Msuva wa Yanga ambaye amefikisha mabao tisa.

Kocha Msaidizi wa Coastal Union, Jamhuri Kihwelu ‘Julio’ amesikitishwa na timu yake kufungwa na mabingwa watetezi, Azam FC, kitendo ambacho kimewadhalilisha kwa kile alichodai kuwa wamefungwa na timu mbovu.

Coastal Union ilifungwa bao 1-0 na Azam juzi kwenye Uwanja wa CCM Mkwakwani.

Julio alisema anashangazwa na mpira wa kiwango cha chini unaochezwa na Azam, ambayo ina kila kitu kuanziamiundombinu na kuwalipa fedha nzuri wachezaji ambao yeye alidai kuwa kiwango chao ni cha chini na hawapaswi kuwa hapo.

“Kinachoniuma ni kufungwa na timu mbovu kama Azam, nashindwa kuelewa wachezaji wa Azam wana matatizo gani hadi wanacheza kwa kiwango cha chini kiasi hiki, Azam ina kila kitu tofauti na hizi timu zetu na kwa mfumo huu sidhani kama wanaweza kufika mbali kisoka.

“Nafikiri hawana mipango mizuri katika usajili ndiyo maana wachezaji waliopo wanashindwa kuipa hadhi klabu yao kwa kuonyesha soka safi, tumefungwa ila wachezaji wangu wameonyesha kiwango kizuri japokuwa nafasi walizozipata wameshindwa kuzitumia kama wenzetu ambao wanabutua butua tu,” alisema Julio.

Kocha wa Azam, George Nsimbe alisema: “Kwa sasa hatutaki kuangalia tunafunga mabao mangapi, kikubwa tunachopigania ni kupata pointi tatu kila mechi na hii ni kutokana kwamba tuna lengo la kutetea ubingwa, mechi zilizobaki tunatakiwa kushinda zote. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

No comments:

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...