Wednesday, March 18, 2015

AL SHABAAB YAUA WATU WATATU NCHINI KENYA

Alshabaab
Maafisa wa polisi nchini Kenya wanasema kuwa takriban watu watatu wameuawa katika mji wa kazkazini wa Wajir, yapata kilomita 100 kutoka mpaka na Somalia. Watu waliofunika nyuso zao walishambulia duka moja na kufyatua risasi, kulirushia magurunedi kabla ya kulichoma.

Kundi la wapiganaji wa Al-Shabaab limeongeza mashambulizi yake kazkazini mashariki mwa Kenya katika siku za hivi karibuni ,na kufanya mashambulizi mawili katika mji wa Mandera ambao una pakana na Somali.

Kundi hilo linadhibiti eneo kubwa la Somalia la mashambani na limesajili idadi kubwa ya raia Wakenya. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

Na BBC

No comments:

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...