Wednesday, August 27, 2014

WANANCHI WAKATAA FIDIA ILI KUJIPATIA UMEME

Displaying Mbunge wa Jimbo la Ludewa, Deo Filikunjombe (mwenye shati la kijani) akifukia udongo kwenye shimo wakati wa kusimamisha nguzo ya umeme kwenye kijiji cha Nindi kwa ajili ya kusambaza umeme vijiji.JPG
Filikunjombe mwenye shati la kijani akishirikiana na wananchi kufukia nguzo 
Displaying Mafundi wa Shirika la Umeme Tanzania wakiwa wamebeba nguzo ya umeme wakipeleka kusambaza kwenye mashimo yaliyochimbwa katika kijiji cha Nindi, Kata ya Lupingu wilayani Ludewa. (Picha na Michael Katona).JPG
Vijana wa TANESCO wakiwa kazini
IMG_5343_f8d22.png
Kazi na dawa Filikunjombe akiwa na kihifadhia chakula (Hot port) lenye karanga baada ya njaa kumkabili
IMG_5294_f599f.png 
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz
IMG_5299_434cd.png
Filikunjombe akichimba shimo
IMG_5308_06c6c.png
Shimo hili lilifika futi sita hilo Filikunjombe akishirikiana na wananchi hadi kuhakikisha nguzo zinasimama

 IMG_5340_56340.png
Wanawake wakazi wa Lupingi wakikata miti nili nguzo ziendelee kupita
IMG_5326_cfa9f.png 
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

IMG_5330_eaf67.png


WANANCHI wa kijiji cha Nindi Kata ya Lupingu wilayani Ludewa wamekubali kuruhusu maeneo yao kutumika kupitisha nguzo za umeme zinazowekwa hivi sasa na Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) bila ya kuidai serikali fidia.
Uamuzi wa wananchi hao kuruhusu kutumika kwa maeneo yao umeadhimiwa mbele ya Mbunge wa Jimbo la Ludewa, Deo Filikunjombe wakati alipoongoza wananchi hao wa kijiji cha Mtumbati kufyeka miti iliyopo kwenye mashamba yao kwa ajili ya kuchimba mashimo ya kuweka nguzo za umeme.


"Iwapo wananchi hao wangekuwa kama wale wa mijini ama mikoa mingine ambao wamekuwa wakikwamisha miradi kuanza kwa wakati kutokana na kudai fidia kwa kila kitu, basi isingewezeka umeme kufika Lupingu, ungechukua muda mrefu zaidi, hasa kutokana na wingi wa miti,mashamba ya mihogo na mali nyingine ambazo zingepaswa kufanyiwa tathimini kabla ya kuondolewa," alisema Filikunjombe.
"Tunamshukuru mbunge kwa jitihada zake hizi anazozionyesha hivi sasa kwenye jimbo letu, tumeshirikiana kwa pamoja kufanya kazi na yeye kwa ajili ya kufyeka na kuchimba mashimo, tumekubaliana hatuoni sababu ya kudai fidia mashamba yetu yalipwe na serikali," alisema Hapiness Kayombo mkazi wa Mtumbati.
Naye Otilia Lukuu mkazi wa Nindi alimpongeza Mbunge Filikunjombe kwa kuwaletea maendeleo ya haraka kwenye kijiji chao hicho, ambapo alidai awali hali ya mawasiliano ya barabara kutoka kijiji cha Nindi kwenda Ludewa ilikuwa ni changamoto kubwa na kwamba hivi sasa usafiri wa basi na gari ndogo umekuwa ukitumiwa na wakazi wa Lupingu wanaofanya biashara ya dagaa na samaki kwenda kuuza mjini Ludewa.
"Tunafurahi kupata hivi sasa barabara ya uhakika ya kupitisha magari, na vilevile ujio wa umeme kwenye kijiji chetu, kila mkazi atakuwa na uhakika wa kupata umeme, hatuoni sababu ya kudai fidia kwenye mashamba yetu," alisema Lukuu.
Mbunge Filikunjombe akiwa kwenye kijiji cha Nindi aliwapongeza wananchi wa kijiji vya Nindi, Mtumbati na Lupingu kuruhusu maeneo yao hayo kutumika kupitisha nguzo za umeme kutoka mjini Ludewa kwenda Kata ya Lupingu bila ya kudai fidia yoyote, jambo ambalo litasaidia kuleta maendeleo makubwa kwenye kata hiyo pindi umeme huo utakapowashwa.
Filikunjombe alisema jitihada anazozifanya kwenye jimbo lake la Ludewa ni sehemu ya kutimiza ahadi zake kupitia Ilani ya uchaguzi ya chama cha Mapinduzi (CCM), ambayo iliahidi kufikisha umeme kila kaya kwa lengo la kuchochea maendeleo kwa haraka katika maeneo ambayo kwa muda mrefu yamekuwa hayapati nishati hiyo ya umeme.
Mbunge huyo ambaye alishirikiana na wananchi hao kuchimba mashimbo, kufyeka miti na kubeba nguzo za umeme, alisema ameridhishwa na kasi inayofanywa na wananchi hao ya kujitolea nguvu zao kuchimba mashimo na kusogeza nguzo katika mashimo hayo,kuwa ni wazi mradi huo wa umeme utakamilika kabla ya mwezi Desemba mwaka huu.
Filikunjombe alisema, wakati akiingia madarakani mwaka 2010 ni Kijiji kimoja pekee cha jimbo hilo la Ludewa ambacho kilikuwa na umeme wa mafuta, lakini hivi sasa zaidi ya vijiji 10 tayari vimepata umeme na kwamba jumla ya vijiji 49 vipo kwenye mpango huo wakufikiwa na mradi wa umeme huo ambao unatekelezwa kwa nguvu za serikali ya Tanzania, Swedeni na Kanisa na Katoliki Dayosisi ya Njombe.
Akizungumzia kasi ya usambazi wa nguzo za inayoendelea hivi sasa ya kupeleka umeme kwenye Kata ya Lupingu, Kaimu Meneja wa Tanesco wilayani Ludewa, Ramadhani Mwanga alisema wanatarajia kuanza kuweka nyaya za umeme kutoka Ludewa hadi kijiji cha Nindi ndani ya wiki mbili zijazo.
"Tupo mbioni kuwasha umeme kwenye vijiji hivi, lakini tumekuwa tukifanya kazi kwa kasi kuhakikisha hadi kufikia mwezi Desemba umemeuwe umeshawaka kwenye vijiji vyote vilivyopo ndani ya kata ya Lupingu," alisema Mwanga. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Na Mathias Canal

No comments:

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...