Wednesday, August 27, 2014

UKRAINE NA URUSI ZAFANYA MAZUNGUMZO

Marais Vladmir Putin wa Urusi(kushoto) na Petro Poroshenko wa Ukraine(kulia) wakikutana Mensk, Belarusse tayari kwa mazungumzo
Marais wa Urusi na Ukraine wamekuwa na mazungumzo ya kwanza ya moja kwa moja kuhusu mgogoro wa eneo la mashariki mwa Ukraine, lakini inaonekana hakuna welekeo wa mgogoro huo. Kiongozi wa Ukraine Petro Poroshenko amesema "mpango" utaandaliwa haraka iwezekanavyo kumaliza mapigano kati ya majeshi ya Ukraine na waasi wanaotaka kujitenga.
Rais Vladimir Putin wa Urusi amesema nchi yake itasaidia katika mazungumzo, lakini suala la usitishaji mapigano ni la Ukaraine yenyewe. Ukraine imekuwa ikiishutumu Urusi kwa kuwapatia silaha waasi, madai ambayo yanakanushwa na Urusi.
Kabla ya mkutano wao wa ana kwa ana katika mji mkuu wa Belaruse, Minsk, viongozi hao wawili pia walishiriki katika mazungumzo na afisa wa ngazi ya juu wa Umoja wa Ulaya, Catherine Ashton.
Mgogoro nchini Ukraine
Mkutano huo unakuja baada ya askari kumi wa Urusi kukamatwa mashariki mwa Ukraine.
Mwanadiplomasia Ashton ameyaelezea mazungumzo yaliyowashirikia viongozi mbalimbali wa Ulaya kuhusu mgogoro wa Ukraine kuwa una mwelekeo"sahihi".
Umoja wa Ulaya pamoja na Marekani zimeiwekea Urusi vikwazo vya uchumi kwa kushindwa kuwadhibiti waasi. Zaidi ya watu 2,000 wameuawa katika mapigano kati ya majeshi ya Ukraine na waasi katika majimbo ya Donetsk na Luhansk.
Majimbo hayo mawili yamejitangazia uhuru kutoka Kiev kufuatia hatua ya Urusi ya kujinyakulia eneo la kusini la Crimea kutoka Ukraine mwezi March 2014.
Mazungumzo kati ya Bwana Poroshenko na Bwana Putin yalidumu kwa takriban saa mbili bila kuruhusu vyombo vya habari. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Na BBC

No comments:

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...