Friday, February 15, 2013

NCCR – Mageuzi yapinga hatua zozote za kutaka kuzuia matangazo ya moja kwa moja kutoka bungeni.

Chama cha NCCR – Mageuzi kimesema kimesema kimepokea kwa masikitiko makubwa taarifa ya Katibu wa Bunge kwa waandishi wa habari juu ya mpango wa kuzuia kurusha matangazo moja kwa moja na badala yake kuyafanyia kwanza uhariri kabla ya kuwafikia walaji.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini dar es Salaam, Kaimu Katibu Mkuu wa chama hicho Faustin Sungura NCCR – Mageuzi inapinga kwa nguvu zote, hatua zozote zinazotaka kuchukuliwa na mamlaka yeyote za kuzuia matangazo ya moja kwa moja kutoka bungeni.
Amesema wanapinga hatua hizo kwa sababu, hoja na sababu za kutekeleza azma hiyo kama zilivyotolewa na Katibu wa Bunge ni hoja dhaifu na hasi.
Amesema mawazo ya Katibu wa bunge yanakinzana na Ibara ya 18(d) ya katiba ya nchi.(Picha na Maktaba).

No comments:

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...