Tuesday, February 26, 2013

Tigo yaongeza kifurushi cha ziada kwenye huduma za Blackberry!

Tigo Tanzania imezindua kifurushi kipya cha Blackberry ambacho kitawapa wateja  fursa ya kutumia mitandao ya kijamii kwa bei nafuu zaidi kijulikanacho kama Blackberry Social Plan.
Kifurushi hiki kitawawezesha wateja wa Tigo kutumia mitandao ya kijamii kama Twitter, Facebook, Whatsaap na mingineyo  ipasavyo kwa gharama nafuu zaidi. Watumiaji wanaweza kujiunga na kifurushi cha siku, wiki au mwezi kutokana  na matumizi yao.
Ndg. William Mpinga, meneja wa chapa ya Tigo alisema kuwa “Mitandao ya kijamii imezidi kuja juu baada ya watumiaji kuongezeka maradufu na kuitumia kwa matumizi mbalimbali kama kutafuta habari, kutumiana ujumbe n.k.  Mitandao hii hupatikana kiurahisi sana bila gharama yeyote hivyo kuifanya idadi ya watumiaji kukua kwa kasi kubwa sana. Watumiaji wa kifurushi cha blackberry watanufaika na huduma mbalimbali muhimu ambazo zitawasaidia kujiendeleza kibiashara na kikazi kwa kuwaweka karibu na wafanyabiashara au wafanyakazi wenzao pamoja na wateja  wao. Huduma kama BBm na Whatsapp zitawawezesha kujadili mambo mbalimbali kama vile wako mahali pamoja hivyo kupunguza haja ya mikutano ya kila mara. Watumiaji wataweza kufanya haya yote wakiwa majumbani kwao, au kwenye mizunguko yao mbalimbali.”
Mr. Mpinga aliendelea kwa kusema kuwa “tuliamua kuzindua kifurushi hiki  ili kuwapatia wateja wetu huduma mbadala juu ya kifurushi cha Blackberry na hivyo kuongeza thamani ya huduma zetu.”
Kutumia huduma hii mteja inabidi ajiunge kwa kutuma ujumbe kwenda 15518 wenye neno BBS1 kutumia kifurushi cha siku, BBS7 kutumia kifurushi cha wiki, na BBS30 kutumia kifurushi cha mwezi.  Gharama za siku ni shilingi 499, za wiki shilingi 2,999 na za mwezi shilingi 11,999. Kwa kutumia kifurushi hiki wateja wataweza kutumia mitandao ya kijamii ipasavyo kabisa.

No comments:

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...