Wednesday, March 21, 2018

MAGUFULI ATENGUA UTEUZI WA KIGOGO WA SHIRIKA LEO MARCH 21


Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Shirika la Nyumba la Taifa (National Housing Corporation – NHC) Bi. Blandina Nyoni.

Taarifa kutoka Kurugenzi ya Mawasiliano Ikulu asubuhi ya leo March 21, 2018 inaeleza kuwa Rais Dkt. John Magufuli ametengua uteuzi wa Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Shirika la Nyumba la Taifa (National Housing Corporation – NHC) Bi. Blandina Nyoni kuanzia leo.

Pia taarifa hiyo inaeleza kuwa Rais Magufuli ameivunja Bodi ya shirika hilo la NHC. Uteuzi wa Mwenyekiti mpya na bodi nyingine utafanyika hapo baadaye. Tunapenda kuwataarifu wadau wetu kuwa hivi karibuni tutapatikana kwa website ya jambotz.co.tz

No comments:

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...