Tuesday, March 27, 2018

BRAZIL KULIPIZA KICHAPO CHA 7-1 AU KUAIBISHWA TENA?!

Brazil full-back MarceloHaki miliki ya pichaJambo tz
Mkufunzi wa Brazil Tite amesema timu yake bado inatatizwa na "mizimu" ya kipigo cha 7-1 ambacho walipokezwa na Ujerumani katika nusu fainali ya Kombe la Dunia miaka minne iliyopita.
Mataifa hayo mawili yatakutana tena mara ya kwanza Jumanne mjini Berlin tangu Brazil walipoaibishwa kwao nyumbani wakati wa michuano hiyo ya Kombe la Dunia.
"Hii ina maana kubwa sana kisaikolojia hakuna anayehitaji kujidanganya kuhusu hilo," Titea aliambia jarida la Kicker.

"Matokeo hayo ya 7-1 ni kama mizimu, watu bado huyazungumzia. Kadiri unavyoyazungumzia zaidi, ndivyo mizimu hii inavyochukua muda mrefu kutoweka."
Toni Kroos alifunga mabao mawili wakati huo naye Miroslav Klose akavunja rekodi ya ufungaji mabao Kombe la Dunia mwaka 2014 Ujerumani walipoafanikiwa kujiweka mbele 5-0 dakika 29 za kwanza kwenye nusu fainali hiyo.
Katika mechi hiyo ya kimataifa ya kirafiki itakayochezewa Berlin, kiungo wa kati wa Manchester City Fernandinho anatarajiwa kuingia uwanjani nafasi ya Douglas Costa.
Hilo litakuwa ndilo badiliko pekee kwenye timu ambayo ililaza Urusi 3-0 mjini Moscow mnamo Ijumaa bila nyota wao Neymar ambaye anauguza jeraha.

No comments:

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...