Tuesday, March 27, 2018

WATU WANNE WAKAMATWA WAKIHUJUMU MIUNDOBINU YA TANESCO MKOANI MBEYA

Meneja wa TANESCO Mbeya akiongea na waandishi wa habari pembeni ni Kamanda wa polisi mkoani Mbeya DCP Mohammed Mpinga.

 Polisi Mkoani Mbeya wamefanikiwa kuwakamata watu wanne kwa tuhuma za kuingilia miundombinu ya shirika la umeme nchini (TANESCO).

Akiongea na waandishi wa habari leo kamanda wa polisi mkoani humo DCP Mohammed Mpinga amesema jeshi hilo kwa kushirikiana na maafisa wa Tanesco march 23, mwaka huu walifanya Oparesheni katika maeneo ya vijiji vya Isebe na Isajilo vilivyopo Wilaya ya Rungwe kufuatia taarifa za siri kutoka kwa raia wema kuwa kuna watu wanaingilia miundombinu ya Tanesco katika vijiji vyao pamoja na kufanya wizi wa nguzo za umeme na kuwaunganishia umeme wakazi wa maeneo hayo kinyume cha sheria. 
Watuhumiwa wa uhujumu miundombinu ya TANESCO wakiwa chini ya ulinzi wa jeshi la polisi.


Amewataja watuhumiwa hao kuwa ni Idd Hamis Mwambusye Mkazi wa Bagamoyo, Benard Kibondi Mkazi wa Kikota, Thobias Wilfred, Mkazi wa Iponjola, Eng. Geofrey Msunga Mkazi wa Mbeya.

Kamanda Mpinga amesema miongoni mwa watuhumiwa hao baada ya kukamatwa na kupekuliwa majumbani kwao walikutwa na vifaa mbalimbali vya umeme ikiwa ni pamoja na Mita za umeme 27, nyanya za umeme mkubwa na ndogo, nguzo 57 za umeme ambazo walikuwa zikitumika kuwaunganishia umeme wananchi pamoja na vifaa vingine.

Watuhumiwa watafikishwa Mahakamani mara tu baada ya upelelezi kukamilika. Pia ameelez kuwa jeshi hilo litaendelea na msako mkali kuwasaka watuhumiwa wengine wanaojihusisha na uhujumu wa miundombinu ya Shirika la Umeme  TANESCO katika maeneo mbalimbali.

No comments:

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...