Monday, October 07, 2013

WASTARA APEWA MGUU WA BANDIA BURE NCHINI KENYA...!!!

STAA wa filamu za Kibongo, Wastara Juma Jumamosi iliyopita alikwea pipa kuelekea nchini Kenya ambako ana ziara ya siku nne kikazi na akiwa humo alipata fursa ya kupewa mguu wa bandia bure na wenyeji wake huku pia akiahidiwa kufanyiwa ‘check-up’ ya mwili mzima.
 
Wastara Juma.
Akizungumza na Ijumaa Wikienda, Wastara alisema kuwa anajisikia furaha kupewa ofa hiyo kutoka kwa wadau wa tasnia ya filamu pande za Kenya ambao wamekuwa wakivutiwa na kazi zake.
“Nimepewa ofa ya mguu bandia wa bure ambao utanisaidia, pia nitafanyiwa uchunguzi wa mwili mzima pamoja na mambo mengine. Nina furaha kwa heshima hiyo niliyopewa na wadau hao na kwa msaada wao huo, Mungu atawalipa,” alisema Wastara.
Enzi za uchumba wake na marehemu Juma Kilowoko ‘Sajuki’ walipata ajali iliyosababisha Wastara kukatwa mguu ambapo aliwekewa wa bandia. hivyo mguu huo aliopewa ni wa pili ili kama atahitaji abalishe ule wa zamani.

No comments:

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...